EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 15, 2012

"Nitaanika kila kitu baada ya siku 40 kuanzia sasa" - Dkt. Ulimboka

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dkt. Stephen Ulimboka, amesema anatarajia kuanika madudu ya watu waliomteka na kumfanyia vitendo vya kinyama, baada ya kufanya uchambuzi wa kina mkasa uliomkumba.

Akizungumza katika mahojiano maalum na MTANZANIA mjini Dar es Salaam jana, Dkt. Ulimboka alisema ataanika madudu yote aliyofanyiwa, baada ya siku 40.

Dkt. Ulimboka, aliyerejea kutoka nchini Afrika Kusini, alikokuwa amekwenda kutibiwa, alisema ana siri nzito moyoni ambayo akiitoa, Watanzania watamuelewa tu.

Alisema baada ya kurudi nyumbani salama, hivi sasa amejikita zaidi kufanya uchambuzi wa mambo au matukio yaliyomsibu kabla ya kupelekwa Afrika Kusini ili ukweli ujulikane.

“Nawaomba Watanzania wawe na subira kwanza, nitaanika kila kitu baada ya siku 40 kuanzia sasa, jambo kubwa ninaloangalia sasa ni kuimarisha kwanza afya yangu ambayo Mungu amenipigania vya kutosha, baada ya hapo nitaeleza kwa kina mkasa huu ulionikuta wakati wa mapambano ambayo nyote mnayajua. Napenda kuwahakikishia Watanzania na madaktari wenzangu, kuwa nitaendelea kusimamia kile ninachoamini na kukitetea…nitaendelea kuongoza Jumuiya ya madaktari, nitaendelea kujiamini ili kuhakikisha tunapigania madai yetu,” alisema Dkt. Ulimboka.

Kuhusu familia yake, kama inaweza kutoa tamko, Dkt. Ulimboka alisema hafahamu iwapo familia imeandaa mpango huo, lakini kwa upande wake, wakati ukifika atalitoa mbele ya umma kama ilivyo kawaida yake kwa ushahidi wa kutosha, “Kuhusu suala la uchunguzi, siwezi kulizungumzia sana kwa sababu kama nilivyosema siwezi kukurupuka kuanza kutoa ushirikiano na Jeshi la Polisi, wakati sijausoma mkasa wenyewe kama unaendelea vipi. Nimesikia baadhi ya vyombo vya habari, vikisema nimefichwa, jamani sijafichwa na familia…. naendelea na shughuli zangu kama kawaida, lakini jambo la msingi ni kuimarisha kwanza afya yangu, kabla ya kuanza kukutana na waandishi wa habari hadharani,” alisema Dkt. Ulimboka na kuongeza, “Nipo kwenye mihangaiko yangu na muda huu nipo safarini, naelekea mjini Bagamoyo.”

Katika hatua ya kushangaza, Dkt. Ulimboka aliamua kutumia usafiri wa boti kwenda Bagamoyo, tofauti na siku ambazo amekuwa akitumia njia ya barabara.

Hii ni mara ya kwanza Dk. Ulimboka kuzungumza kwa kina na MTANZANIA, tangu aliporejea kutoka nchini Afrika Kusini, ambako alikwenda kutibiwa Juni 27, mwaka huu.

Wakati Dkt. Ulimboka akisema hayo, ofisa mmoja wa Jeshi la Polisi nchini, ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, aliiambia MTANZANIA kuwa, hivi sasa jeshi hilo linaendelea na vikao ili kuona ni namna gani wanaweza kushughulikia suala la Dkt. Ulimboka.

Habari za kuaminika kutoka kwa ofisa huyo, ni kwamba Ijumaa wiki hii linaweza kutoa ufafanuzi zaidi au hatua zitakazochukuliwa dhidi ya daktari huyo.
Na Gabriel Mushi, Gabriel Masese via gazeti la MTANZANIA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate