Mmoja wa wanadada (mwenye suti) waliokuwamo ndani ya gari akifarijiwa. Mwenzake alikimbizwa Marie Stopes kwa kwa huduma ya kwanza
Na: Rodrick Maro
Japo inasemekana kuwa ajali haina kinga, ila tahadhari ni muhimu. Barabara inayounganisha Shekilango na Alli Hassan Mwinyi, eneo la Sayansi, lipo katika matengenezo.
Hivyo, inapaswa madereva kuchukua tahadhari, kwani barabara hiyo haijakamilika na pia mkandarasi yupo kazini.Bahati mbaya sana, asubuhi hii, majira ya saa Moja, wanadada wawili wamejikuta gari lao, Escudo likigeuka lilikotoka na kuwa miguu juu, mbele kabisa la Jengo la Kituo cha Sheria na Haki za Biandamu (Justice Lugakingira House)! Ila la kumshukuru MUNGU ni kuwa wamepona, japo hawakuepuka michubuko midogo midogo.
Chanzo cha habari ni mjengwablog.
No comments:
Post a Comment