MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Jakaya Kikwete amesema
kwamba migogoro ndani ya chama hicho inasababishwa na uroho wa vyeo na
madaraka kiasi cha kusababisha vita kubwa ndani ya CCM.
Akizungumza na Wanachama CCM katika Mkutano Mkuu wa Nane wa chama
hicho unaoendelea mjini Dodoma alisema, kuna watu hodari wa kuwachukia
wenzao kwa sababu tu wamekataa kuwaunga mkono ama wamekataa kuwaunga
watu wao mkono..
“Migogoro ndani ya CCM inasababishwa na uroho wa madaraka,kwanini
mgombane kwa kugombea uongozi, kwanini mtu achukiwe kwa kugombea
uongozi, kwanini afanyiwe vitimbi, kwanini umchukie mtu aliyeamua
kumuunga mkono mgombea mwingine, na kwanini umchukie aliyekataa kukuunga
mkono wewe au kwa sababu amekataa kumuunga mkono mtu unayemtaka,
tukiacha hayo hakuna mgogoro mwingine ndani ya chama niambieni”alisema
Rais Kikwete na kuhoji.
Nape akitumbuiza
Alisema “viongozi wenye chuki na bivu kubwa ndani ya Chama hicho
ndiyo wenye tabia ya kuwa na andimi mbili na kiongozi mwenye ndimi
mbili hawafai ndani ya CCM kwa sababu akigeuka huku anasema ya CCM
akigeuka huku anasema ya wengine, hivyo kuwa viongozi hao ndani ya CCM
nisawa na kufuga nyoka ndani ya nyumba au mfukoni ambaye ukiingiza mkono
tu mfukoni anakung’ata, bali tunataka kiongozi muadilifu na mwenye
kuitendea haki chama na kutetea maslahi ya chama na mwenye uelewa mpana
wa mambo ya chama”.
Katika hatua nyingine Rais Kikwete aliongeza kwamba uchaguzi wa
viongozi uliopita katika Chama hicho ulikuwa na changamoto zake ambazo
hawakuzizoea na wala hawakujiandaa kukutana nazo.
“Uchaguzi wa viongozi uliopita ndani ya CCM ulikuwa na changamoto
ambazo hatukuzizoea na hatukujiandaa kukutana na nazo hivyo tukajikuta
tuna wakati mgumu wa kufanya maamuzi yetu ya viongozi wetu lakini
tumejifunza kutokana na hayo na tusikubali yajirudie katika chaguzi
zetu”alifafanua Rais Kikwete.
No comments:
Post a Comment