EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, November 19, 2012

Kivuli cha Chadema chaitisha CCM.

Na Mwandishi Wetu
KIVULI cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kinaonekana kukitisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya jina la chama hicho kutawala katika mkutano mkuu wa CCM uliomalizika Jumanne mjini Dodoma.
Jina la Chadema lilianza kutawala katika mkutano huo, Jumapili Novemba 11 mwaka huu, wakati makada wa chama hicho waliokuwa wakigombea ujumbe wa Halmashauri Kuu (Nec), wakijinadi kwa wajumbe.
Chadema ilitumiwa na baadhi ya wagombea wa nafasi 10 za Bara na Visiwani kama kete yao ya kuchaguliwa kupata nafasi hiyo.
Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (MSZ) Dk Ali Mohamed Shain akisalimiana na wanachama wa CCM
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira wakati akiomba kura aliwaambia wajumbe wa mkutano huo wampe kura ili apeleke kilio Chadema.
Alisema akichaguliwa mjumbe wa Nec atapata nguvu ya kupambana na Chadema.
“Nipeni kura ili nipate nafasi nipeleke kilio Chadema,” alisema Wassira huku akishangiliwa wakati akiomba kura na Rais Jakaya Kikwete akimwita kwa jina la utani ‘Tyson’.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa chama hicho, (UVCCM), Martine Shigela wakati akiomba kura kwa wajumbe wa mkutano huo alisema yeye ndiye anayeongoza jeshi la ardhini linalopambana na wapinzani wanaopiga kelele.

“Mimi ndiye ninayeongoza jeshi la ardhini linalopambana na wapinzani wanaopiga kelele,” alisema.
Naye Mwanamanga Manguga aliwaomba wajumbe wampigie kura ili CCM aipeleke Chuo Kikuu cha Dodoma anakosoma na kwamba, tayari ameshaingia katika mapambano.
Alisema katika uchaguzi wa udiwani uliopita Kata ya Msalato mjini Dodoma, wafuasi wa Chadema walimpiga mawe na kumjeruhi wakati akitetea chama hicho.
Chadema pia ilikuwa ikitamkwa sana na mshereheshaji wa mkutano huo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho Nape Nnauye wakati akitoa matangazo mbalimbali kwa wajumbe. 

“Watawezaaa… Wataweza hao Chadema…,” alisikika akiwaambia wajumbe wa mkutano huo nao wakimjibu; “Hawaweziii!”
Vilevile, Chadema ilikuwa ikitajwa sana na wapambe wa wagombea wa nafasi ya Nec ambao mara kwa mara walisikika wakiwaambia wachague wagombea wao kwa sababu ndio wenye uwezo wa kupambana na Chadema.
Mpambe mmoja wa mgombea mmoja ambaye hakupenda kutajwa jina lake, aliliambia Mwananchi Jumapili kuwa chama hicho kinapaswa kuchagua safu ya uongozi ambayo itakuwa ni mwiba kwa Chadema.

Hata Rais Jakaya Kikwete wakati akifunga mkutano huo, Novemba 13 mwaka huu, aliwataka wanachama wa chama hicho kuwajibu wapinzani kwa hoja, kama alivyofanya, aliyekuwa Katibu wa Uchumi na Fedha wa chama hicho, Mwigulu Nchemba wakati wa Bunge la Bajeti mwaka huu.
Alisema, “Baada ya wapinzani kutoa bajeti yao, kijana wetu, Mwigulu alisimama akaivunjavunja bajeti yao. Wakanywea. Ndivyo tunavyopaswa kufanya.
Chanzo Mwananchi

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate