EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, December 12, 2012

Rayuu Aingia Matatani Tena-Sasa Mume wa Mtu.

MSANII wa filamu na tamthilia bongo Rayuu, inadaiwa kuwa amenusurika kupelekwa polisi na mwanamke mmoja kwa madai kuwa alikuwa akitembea na mume wake, huku pesa nyingi za matumizi zilikuwa zikienda kwa msanii huyo.

Wiki iliyopita hali ilikuwa ngumu kwa msanii huyo kwani taarifa za kupelekwa polisi zilimpa wakati mgumu hadi kuchukua hatua ya kujifungia ndani ili kupumzika na kupisha taarifa hizo ambazo zingemchafua pengine hata kujiigiza kwenye matatizo makubwa.

Chanzo kimoja kilichozungumza  kilidai kuwa msanii huyo alikuwa akitembea na jamaa huyo bila kujua ni mume wa mtu huku wakitanua sehemu tofauti tofauti za starehe.Hata hivyo taarifa hizo za kuonekana sehemu kadhaa na jamaa zilimfikia mke huyo anayedaiwa kuwa mke wa jamaa, ndipo alipotafuta namba ya simu ya Rayuu na kumtaka aachane na mume wake mara moja bila hivyo anaweza kumfikisha kituo cha polisi na akajibu mashtaka.

“Wiki iliyopita tu huyo mwanamke baada ya kupewa taarifa kuwa mume wake anakula bata na msanii huyo, ndipo alipoamua kuchukua maamuzi ya kumpigia simu Rayuu ili kumwambia achane na mume wake,” kilisema chanzo hicho.

Hata hivyo mwandishi alimtafuta Rayuu ili kuzungumzia ishu hiyo, ambapo alidai kuwa alipigiwa simu na mwanamke huyo ya kumtaka achane na mume wake, lakini awali kabisa hakujua kama ni mume wa mtu.

Alisema hakuwa na makosa kwani jamaa alipomfuata hakusema kuwa ni mume wa mtu na wala hakuwa na ishara zozote zinazoonesha ana mke nyumbani na muda wote alipomtafuta walikuwa wakionana na kufanya yote kama wapenzi.

“Sikujua kama ni mume wa mtu na nimekuwa naye katika mahusiano kwa muda mrefu lakini nilipatwa na mshtuko baada ya mwanamke anayedaiwa kuwa mke wa jamaa huyo kunipigiwa simu tena kwa matusi na kudai kuwa nikae mbali na mume sikujua anazungumzia nini lakini baada ya muda jamaa mwenyewe akaniweka wazi kuwa ni mume wa mtu,” alisema Rayuu.

Alipoulizwa swali kuwa baada ya kujua jamaa ni mume wa mtu alichukua hatua gani, alidai kuwa hakuwa na kitu cha kufanya zaidi ya kuachana na jamaa kwani hataki yaje kumkuta makubwa zaidi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate