EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, January 17, 2013

KUMNYENYEKEA MWENZA WAKO SIYO UBWEGE NI CHACHANDU YA NDOA

MADA ya leo inawagusa walio katika ndoa na wale wanaotarajia kuingia. Unapoingia kwenye ndoa kitu cha kwanza ni kufikiria jinsi ya kuilinda kwa gharama yoyote. Kuingia kwenye ndoa na kutoka baada ya muda mfupi ni kujitafutia gundu lisilo na sababu.
Tunapogeukia suala la ulinzi wa ndoa yako sasa, hivi utashindwa kweli kumnyenyekea mpenzi wako? Unatashindwa kumvumilia mpenzi wako eti kwa sababu utajihisi wewe ni mtumwa wa mapenzi? Mathalani mkeo anaumwa na kwa bahati mbaya hamna msichana wa kazi, je utashindwa kumsaidia kazi kama kupika, kufua, kuosha vyombo na kazi nyinginezo kwa sababu tu wewe ni mwanaume? Hii siyo sawa jamani.

UNYENYEKEVU...
Watu wamekuwa wakilitafsiri tofauti neno hilo wakidhani eti kumnyenyekea mtu ni kuonesha ubwege uliopitiliza. Jamani kama mlikuwa hamjui, kumnyenyekea mumeo, mkeo ni moja ya chachandu ya ndoa. Bila kunyenyekeana hakuna mahaba na mahaba yanapokosekana ndoa haiwezi kuwepo.
Hivi usipomnyenyekea laazizi wako unataka ukamnyenyekee nani? Mumeo/mkeo ndiyo wa kumnyenyekea siku zote za uhai wako. Ndoa kubembelezana bwana, mpenzio akija na mawazo yake, mtu amemuudhi kazini hapo ndipo mahali haswa anapopaswa kumnyenyekea na kumrudisha katika hali nzuri.

Wewe ndiye unapaswa kumsahaulisha kabisa mambo yote yaliyotokea kazini. Mpokee kwa upole, mwambie pole, mkaribishe chumbani kisha mvue nguo zake na umpeleke bafuni mwenyewe. Anza kumwogesha bila kuzungumza naye maneno mengi.
Baada ya hapo mkaushe kwa taulo kisha mrudishe chumbani, mtolee nguo za usiku kisha mpeleke mezani kwa chakula. Baada ya hapo sasa mkiwa sebuleni mnaangalia TV muulize kwa upole: “Dear vipi, mbona leo naona siyo kawaida yako? Umechokachoka...kuna nini mpenzi wangu?”
 
Nakuhakikishia kwamba, kwa kauli kama hiyo hata kama alikuwa na tatizo kubwa anaweza kukujibu; “Ah kuna mtu aliniudhi kidogo ofisini lakini baada ya kufika hapa nyumbani najisikia amani sasa,” tena wakati anakuambia hivyo unaweza kushangaa hata uso wake unaanza kukunjuka. Hiyo ndiyo ndoa jamani.

KUVUMILIANA PIA MUHIMU...
Maisha ya ndoa yanahitaji uvumilivu wa hali ya juu la sivyo siku mbili tu unaweza kuomba talaka kama siyo mwanaume kumkimbia mke. Ndoa ina mambo mengi sana, kutunza familia, kupeana haki za ndoa, kusaidiana na kuvumiliana katika vipindi vya dhiki na faraja na mengineyo.
 
Ukarimu, uaminifu, upendo wa kweli ni kati ya chachu za kudumisha ndoa na kwa kufanya hivyo haiwezi kuwa na migogoro isiyokuwa na lazima.
Unapooa au kuolewa lazima ufahamu kuwa unakuwa umejenga undugu baina ya familia yako na ya mwenzio. Katika kuishi kwenu huko utakutana na matabaka mengi, watu hutofautiana tabia.
 
Mfano wewe mwanamke umeolewa, mumeo akaleta ndugu, yaani wifi zako. Unatakiwa kuwasoma tabia ili uweze kuendana nao.
Ili kufanikiwa katika hili unapaswa kuwa na busara, uvumilivu, unyenyekevu na kuonyesha kuwajali, hii inaweza kukusaidia sana kwani watakapokutendea mambo ya ajabu nawe ukaanza kuwaropokea, utakuwa unajiingiza kwenye migogoro ambayo mwisho wake huweza kuwa mbaya zaidi kwako kuliko kwao.
 
Kumbuka Mungu ametuumba kila mtu na udhaifu wake, ndiyo maana unaona wanandoa wengi wanajikuta wakizikimbia ndoa zao kwa kutendwa na wandani ama ndugu wa wandani wao, wakati mwingine mume anaweza kuwa hajui, unayepaswa kumweleza ni wewe na unapomweleza lazima uzingatie heshima na busara ambayo haitaonyesha umedharau ukoo wao.
 
Siyo unaanza kusema; “Nyoo! Umeniletea ukoo wenu hapa, chakula hakitoshi! Nitawafukuza!” Kwa kauli hiyo utaonekana limbukeni, kaa naye chini zungumza naye kwa ukarimu, mweleze ni jambo gani linakunyima uhuru.
Usimfiche, mwambie; “Mume wangu, kuna jambo wifi amenitendea sijui kama anaona ni kosa lakini mie naona amenikosea, mweleze asirudie tena,” tena hakikisha wakati unamweleza hayo mpo peke yenu chumbani na huenda ni baada ya kumpa haki yake. Upo hapo?
 
Huo ndiyo uvumilivu ninaouzungumzia, siku zote wewe ndiye unayetakiwa kuwa na uchungu na ndoa yako. Kabla ya kuzungumza jambo lolote fikiria mara mbili, halitasababisha matatizo kwako? Ukipata matatizo au kuachika huyo wifi yako atakuwepo? Jibu ni hapana!
Kaa chini, fikiria kwa makini kabla ya kuamua jambo lolote linalohusu ndoa yako. Kumbuka kuwa kuingia kwenye ndoa ni kazi ngumu lakini kazi ngumu zaidi ni kuhakikisha unailinda.

Kwa leo nilitaka kuzungumzia hayo tu nikiamini kwamba ukiyazingatia wewe uliye katika ndoa yatakuwa ni yenye manufaa makubwa kwako.
                                                        Via Global Publishers

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate