Baadhi ya magari yaliyoangukiwa na ukuta.
Gari aina ya Noah likiwa limegandamizwa na zege.
Magari mbalimbali yakiwa chini ya kifusi.
Hii ndiyo hali halisi ya tukio lilivyokuwa.
Gari aina ya Toyota likiwa limebonyezwa na zege.
Ilikuwa ni hasara tupu.
Hali ilikuwa ni mbaya katika zahama hiyo ya alfajiri ya leo.
Watu wakiangalia magari yao.
Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo.
SEHEMU ya ukuta wa kituo cha mabasi ya
kwenda mikoani cha Ubungo, jijini Dar es Salaam, leo alfajiri umeanguka
na kuyaharibu vibaya magari zaidi ya ishirini yaliyokuwa yameegeshwa
nje ya eneo hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela alisema kuwa idadi ya magari yaliyopatwa na ajali hiyo yanakadiriwa kufikia 24 ambapo watu watatu wanasemekana wamejeruhiwa.
Habari/Picha: Musa Mateja/GPL
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela alisema kuwa idadi ya magari yaliyopatwa na ajali hiyo yanakadiriwa kufikia 24 ambapo watu watatu wanasemekana wamejeruhiwa.
Habari/Picha: Musa Mateja/GPL
No comments:
Post a Comment