EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, February 13, 2013

Polisi waanza kuwafuatilia waliomtukana Spika

POLISI mkoani Dar es Salaam wametangaza kuwafuatilia, kuwasaka na kuwachukulia hatua wote waliotuma ujumbe wa matusi ama kupiga simu ya vitisho kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda.
                                              Spika wa Bunge,Anne Makinda 
Viongozi wa Chadema walifanya mkutano wao mwishoni mwa wiki kwenye Viwanja vya Mwembe Yanga, Temeke, jijini Dar es Salaam na kutoa namba za Spika wa Bunge ili mashabiki wamshinikize ajiuzulu.
Pia viongozi hao walitoa namba za simu za Naibu Spika, Job Ndugai ili naye ashinikizwe ang’oke katika nafasi yake kwa madai ya kukandamiza upinzani bungeni.

Chadema walidai kuwa Makinda na Ndugai wamekuwa wakipindisha kanuni wakati wa kuliongoza Bunge. Pia walidai kuandaa taarifa ya kutokuwa na imani na maspika hao, ripoti ambayo wataiwasilisha kwenye Bunge lijalo.

Wakati Polisi wakitangaza hayo, juzi Ofisi ya Bunge kupitia kwa katibu wake, Thomas Kashilillah ilisema itawachukulia hatua kali wale wote waliotumia lugha chafu kwa ujumbe mfupi ama kupiga moja kwa moja kwa Spika na Naibu wake.

Hatua hiyo ya polisi inachukuliwa baada ya Makinda kudai kuwa ametumiwa ujumbe mfupi zaidi ya 400 na kupigiwa simu zisizopungua 200, zinazomkashifu na nyingine zikiwa ni za vitisho dhidi yake.

Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Ahmed Msangi alisema Polisi watafanya uchunguzi kuwabaini wote waliohusika kufanya hivyo na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao ili iwe fundisho kwa wengine.

Msangi alisema kuwa taarifa hizo wamezipata jana na walijipanga kuhakikisha wahusika wote wanatiwa mbaroni.

“Polisi tumeanza kuwafuatilia waliomtukana Spika na lazima tuwakamate kwani kitendo hiki ni kinyume cha sheria,” alisema Msangi.
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake jana, Kaimu Ofisa Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Semu Mwakyanjala alisema suala la vitisho kwa mtu yeyoye linahusu hasa Jeshi la Polisi na kwamba wao ndio wanaopaswa kuchukua hatua zaidi za kisheria.

Wanachama wa CCM Mkoa wa Iringa, wamelaani vikali kitendo cha baadhi ya wafuasi wa Chadema kutuma ujumbe mfupi wa simu za mkononi kumkashifu Makinda huku baadhi yao wakipendekeza chama hicho kifutwe kwa kukosa ustaarabu.

Katibu wa Baraza la Wazee wa CCM Wilaya ya Iringa, Said Mdota alisema kitendo alichofanyiwa Spika Makinda si cha kiungwana na hakikubaliki na wapenda amani wote. Mdota alipendekeza wahusika wote wasakwe na wachukuliwe hatua kali za kisheria.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya wa Wanawake Mkoa wa Iringa, UWT, Zainab Mwamwindi alisema jumuiya hiyo inatarajia kukutana kesho pamoja na agenda nyingine itajadili suala hilo na kulitolea tamko.

“Sisi kama wanawake na Spika ni mwanamke, suala hili limetudhalilisha sana na katika hili tunalikemea kwa nguvu zote na Februari 14, tunatarajia kufanya kikao cha Kamati ya Utendaji tutalijadili na kulitolea tamko,” alisema.

 Naye Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi Mkoa wa Iringa, Ally Simba aliomba vijana kushikamana kukemea tabia hiyo kwani si jambo jema kuona kiongozi wao akidhalilishwa.

Imeandaliwa na Aidan Mhando Dar, Geofrey Nyang’oro na Zainab Maeda, Iringa

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate