EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, February 15, 2013

Waislamu wagongana kuhusu Sheikh Ponda

BARAZA la Habari la Kiislamu (BAHAKITA), limewataka Waislamu nchini kutofanya maandamano yaliyotarajiwa kuanza leo na kesho, kwa lengo la kushinikiza mahakama kutoa dhamana kwa Sheikh Ponda Issa Ponda.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa BAHAKITA, Said Mwaipopo, alisema BAHAKITA kwa kushirikiana na taasisi ya Islamic Peace Foundation, hawaungi mkono maandamano hayo yaliyoratibiwa na Shuhura ya Maimam.

“Tunawataka Waislamu wote nchini wajiweke kando kabisa kuhusu maandamano hayo yanayoratibiwa na Shuhura ya Maimum, kwani hayana kibali chao polisi. Sisi hatuungi mkono kwani wanatakiwa kufuata sheria za nchi,” alisema Mwaipopo.

Mwaipopo alisema, Serikali na Mahakama wanajua wanachofanya, hivyo hawawezi kuendeshwa kwa shinikizo la watu wachache wanaotumiwa na wanasiasa kwa faida zao binafsi.

“Sisi hatufurahii kuona Ponda yuko ndani, ila tunachokitaka ni Waislamu wenzetu wafuate sheria, maana sisi tuna mpango wa kwenda kuzungumza na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi, mratibu wa maandamano hayo achukuliwe hatua kwani ni mtu anayetumika kuchafua hali ya hewa ya nchi,” aliongeza.

Naye Mwenyekiti wa Peace Foundation, Sadi Godogodi, alisema hawaungi mkono maandamano hayo kwani ni kinyume cha sheria. Alisema maandamano hayo yanawaonesha Waislamu kuwa ni watu wa fujo na wasiotaka kufuata utawala wa sheria.

Wakati huo huo, Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limewataka Waislamu kuwa watulivu na kutotumia nguvu kwa hali yoyote katika matatizo yanayogusa hisia za kiimani.
Taarifa hiyo ilitokana na kikao maalumu cha Baraza la Ulamaa chini Mwenyekiti wake, Mufti Sheikh Issa Bin Shabani Simba, kujadili vurugu za Waislamu na Wakristo katika Kijiji cha Buseresere, wilayani Chato mkoani Geita.

Baraza hilo limepokea taarifa hiyo kwa masikitiko na kutaka Waislamu kuwa wavumilivu na kutafuta njia bora ya kuweza kupata mwafaka kutatua mgogoro huo.
Baraza hilo litatuma ujumbe wake haraka kwenda Buseresere kufuatilia mambo yaliyojitokeza ili kupata ukweli uliosababisha vurugu hizo na kuchukua hatua kurejesha amani baina ya Waislamu na Wakristo.


No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate