EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, February 15, 2013

Serikali yaajiri walimu wapya 26,537


WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imetoa ajira mpya kwa walimu 26,537 wa shule za msingi, sekondari na vyuo vya ualimu nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa wizara hiyo, Dk. Shukuru Kawambwa, alisema kuwa utoaji wa ajira hizo haukufanyika kiholela bali ulifuata tathmini mbalimbali zilizofanyika kubaini maeneo yenye upungufu wa walimu ili kuwezesha kupeleka walimu kwa wingi katika maeneo hayo.

Waziri Kawambwa alisema kwa sasa taifa lina upungufu wa walimu wa masomo ya Sayansi na Hesabu na mwaka huu, wameajiri walimu 2,037.
Kwa mujibu wa Waziri Kawambwa, wameajiri walimu 13,568 wa ngazi ya cheti ambapo walimu 13,527 wamepangwa katika shule za msingi zilizopo kwenye halmashauri na 41 wamepangwa katika shule za mazoezi zilizo chini yake.

Alisema kwa upande wa wahitimu wa elimu ya shahada na stashahada, wameajiri walimu 12,893 kufundisha shule za sekondari zilizoko chini ya halmashauri, 59 wamepangwa kuwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu, huku walimu 21 wamepangwa kufundisha shule za sekondari za mazoezi.

Aliongeza kuwa idadi hiyo ya walimu wenye shahada inajumuisha walimu 188 wa elimu maalumu ambao wamepangwa katika shule za sekondari na vyuo vinavyotoa elimu hiyo na kusema kuwa idadi ya walimu walioajiriwa mwaka huu imeongezeka kwa asilimia 11 sawa na walimu 2,630, ikilinganishwa na walimu 23,907 walioajiri mwaka uliopita.
Waziri huyo alisema kati ya walimu wa sekondari na vyuo waliochaguliwa, walimu 1,286 ni wale walioomba ajira serikalini kutoka soko la ajira ambao ni tofauti na wale wanaotoka vyuoni wakati walimu 841 walioshindwa mitihani mwaka jana, wamepatiwa ajira baada ya kurudia mitihani yao na kufaulu.
Alisema orodha ya majina na halmashauri walizopangwa, zinapatikana katika tovuti ya Wizara ya Elimu huku akitoa agizo kwa walimu waliohitimu ambao ni waajiriwa kurudi katika vituo vyao walivyokuwa wanafanyia kazi kabla ya kwenda masomoni.
Waziri Kawambwa alisema walimu wapya wanatakiwa kuripoti katika vituo vyao vya kazi Machi mosi hadi Machi 9, mwaka huu ambapo orodha ya mishahara yao ya mwezi huo itaingizwa katika utaratibu wa serikali.
“Walimu hao lazima waripoti ndani ya muda uliopangwa ili kuondoa usumbufu wa ulipaji mishahara na atakayeshindwa kufika, atakuwa amejitoa kwenye ajira hiyo,” alisema.
Alisema katika ajira hizo walimu wasishangae kupangiwa maeneo ambayo hawajayachagua kwani uteuzi wao umelenga maeneo yenye uhitaji zaidi huku akitolea mfano Mkoa wa Lindi ambao walimu wengi hukataa kwenda huko.
“Tumepanga kulingana na uhitaji, huwa tuna weka mwalimu mmoja kwa wanafunzi 46 lakini kwa hapa Dar es Salaam kuna walimu wengi na kufikia uwiano wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 20,” alisema.


No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate