EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, February 14, 2013

Wanafunzi kuandamana kupinga kidongo chekundu kuwa maegesho

SAKATA la uwanja wa wazi wa kidongo chekundu kubadilishwa matumizi lachukua sura mpya baada ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Dar es Salaam na Shule ya Msingi Gerezani kupanga kuandamana ili kushinikiza kurudishiwa kiwanja hicho.

Miezi michache manispaa ya Ilala walioutupia lawama uongozi wa manispaa hiyo kwa kukigeuza kiwanja cha Kidongo Chekundu kuwa eneo la kuuzia magari.

Wakizungumza  baadhi ya wanafunzi wanaosoma katika shule hizo zilizoko jirani na kiwanja hicho, walidai kushangazwa na hatua iliyofikiwa na uongozi wa manispaa hiyo kuamua kukifanya kiwanja hicho kuwa sehemu ya kuuzia magari chakavu.

Mwanafunzi aliyejitambulisha kwa jina moja la Mussa, alisema kuwa wamechoshwa na ufisadi unaofanyika katika manispaa hiyo hivyo wanalazimika kuandaa maandamano yatakayoelekea katika ofisi ya mkuu wa mkoa ili kushinikiza kuondolewa kwa magari hayo.

Alisema kuwa kutokana na kukosa eneo la kufanyia mazoezi na huku baadhi ya wanafunzi wasichana wakidai kupata vishawishi vya kimapenzi kutoka kwa watu wanaokaa katika eneo hilo ni muhimu suala hilo likapata utatuzi.

“Tunataka kujua wanakusanya kiasi gani maana kama faida ipo ni muhimu ikagawanywa kwa shule zilizopo jirani kuliko faida kutumiwa na watu wachache ambao wamegeuza eneo hilo kuwa mradi wao,” alisema.

Naye Asha Aidy, alisema kuwa sasa hivi wanaogopa hata kupita eneo hilo kutokana na kuwepo kwa vitendo vya vishawishi vinavyotoka kwa watu wanaouza magari hayo.
Alisema kuwa manispaa hiyo ina maeneo mengi ya kuweka maduka ya magari chakavu na sio kukitumia kiwanja hicho ambacho ni mahususi kwa shughuli nyingi za kijamii.
Hata hivyo, gazeti hili lilijaribu kumtafuta diwani wa eneo hilo, Salum Bisarara (CCM), ili kupata kauli yake, ambapo alikiri kuwepo kwa maegesho ya magari lakini alitaka kuiuliza manispaa ndiyo yenye kujua ukweli.

Akizungumza kuhusu malalamiko hayo, ofisa mahusiano wa manispaa hiyo, Tabu Shaibu, alisema kuwa hana taarifa za kuwepo kwa maandamano hayo lakini alikiri uamuzi wa kuweka maegesho wa magari ulifikiwa na manispaa hiyo.
Alisema kuwa manispaa ilianza kukusanya mapato tangu Desemba mwaka jana kupitia maegesho hayo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate