EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, March 15, 2013

Cheyo, Zitto ngoma nzito

Dar es Salaam. 
Hatimaye Bunge limetangaza mabadiliko ya wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge zinazotarajiwa kuanza kukutana kuanzia Jumatatu ijayo, huku baadhi ya vigogo wakiwekwa katika kamati moja na kufanya zoezi la kuchagua wenyeviti wa kamati hizo kuwa gumu.
 
Uteuzi wa majina ya wajumbe hao unakuja mwezi mmoja tangu kumalizika kwa Mkutano wa 10 wa Bunge ambapo, Spika wa Bunge, Anne Makinda alitangaza mabadiliko ya kamati hizo, huku akiifuta Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) iliyokuwa ikiongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.

Kutokana na mabadiliko hayo, shughuli za POAC sasa zitafanywa na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC).

Kamati nyingine iliyofutwa ni ile ya Sheria Ndogo wakati zimeundwa kamati mpya za Bajeti, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na ya Ulinzi na Usalama.
Majukumu ya Kamati ya Bajeti ni kufuatilia utekelezaji wa Bajeti ya Serikali na sera za fedha pamoja na kuainisha na kupendekeza vyanzo vya mapato ya Serikali na kufuatilia mwenendo wa uchumi.
Wajumbe waliokuwepo POAC ambao wamehamishiwa PAC ni Zitto Kabwe, Deo Filikunjombe, Ester Matiko, Zainab Kawawa na Kheri Ali Khamis.
Kamati ya PAC ni lazima iwe na mwenyekiti kutoka kambi ya upinzani, hali inayofanya uchaguzi wake kuwa mgumu kwa kuwa Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP), John Cheyo naye ni mjumbe wa Kamati hiyo.

Cheyo anatazamiwa kupata upinzani mkali kutetea kiti chake kwani atapata upinzani mkali kutoka kwa Zitto, ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya POAC.
Kuna tetesi tayari kuwa Zitto, ambaye alilalamikia kitendo cha kuvunjwa kwa kamati ya POAC, ameanza kampeni za chinichini ili kumtoa Cheyo, ambaye ameshikilia nafasi hiyo tangu mwaka 2005.

Wengine ambao walikuwa wajumbe wa POAC ambao wamehamishiwa Kamati ya Nishati na Madini ni Jerome Bwanausi na Murtaza Mangungu, pia katika kamati hiyo ya Nishati na Madini kuna wajumbe wapya ambao ni Anne Kilango na David Silinde.

Wengine waliokumbwa na mabadiliko hayo ni Grace Kiwelu ambaye amehamishwa kutoka Kamati ya Miundombinu kwenda Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira sambamba na John Mnyika na Ester Bulaya.

Mbunge wa Vunjo (TLP), Augustino Mrema ambaye awali alikuwa mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) ametupwa katika kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, pia Kamati ya Ulinzi na Usalama.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Brigedia Mstaafu Hassan Ngwilizi akibaki katika kamati hiyo, pia yuko katika Kamati ya Ulinzi na Usalama ambayo imemegwa kutoka katika Kamati ya Mambo ya Nje ambayo hivi sasa inaitwa Kamati ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Aliyekuwa mwenyekiti wa Kamati hiyo kabla ya kugawanywa, Edward Lowassa pamoja na makamu wake Mussa Azzan Zungu wamekuwa wajumbe wa Kamati ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Katika uteuzi huo Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia, amekuwa mjumbe wa Kamati ya Kanuni za Bunge na Kamati ya Bajeti, huku Andrew Chenge, Tundu Lissu, Christopher Ole Sendeka pamoja na Zungu wakiwa katika Kamati ya Kanuni za Bunge.
Aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa LAAC, Iddi Azzan amepelekwa katika Kamati ya Masuala ya Ukimwi.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe ambaye awali alikuwa mjumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi, sasa amekuwa mjumbe wa Kamati ya Uchumi, Viwanda na Biashara ambayo imeunganishwa na kuwa moja.Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Selemani Zedi amepelekwa LAAC, huku aliyekuwa mjumbe wa kamati hiyo, Godfrey Zambi akipelekwa kuwa mjumbe wa Kamati ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
Orodha hiyo inaonyesha kuwa kuna Kamati 17 ikilinganishwa na 18 za awali.
Tayari kampeni za chinichini zimeshaanza kwa baadhi ya wabunge ambao wangependa kuwa wenyeviti wa kamati hizo mpya, ambapo wabunge wa CCM jana walitarajiwa kukutana katika Ukumbi wa Karimjee kwa ajili ya kupanga mikakati ya kuchagua wenyeviti wa kamati hizo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate