EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, March 15, 2013

Waziri Membe akanusha kuhusika tukio la kumdhuru Mhariri Kibanda

Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amekanusha madai ya kuhusika na vitendo vya kikatili alivyofanyiwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda.

 
Juzi gazeti la Mtanzania linalochapishwa na Kampuni ya New Habari 2006 Ltd, lilitoa habari inayomtuhumu Waziri Membe kuhusika na uhalifu huo, huku ikinukuu kauli zake alizotoa katika kipindi cha televisheni moja Julai mwaka jana, aliposema ana maadui kumi na moja kati yao wamo waandishi wa habari wawili.

Usiku wa kuamkia Machi 6, mwaka huu, Kibanda akiwa anarejea nyumbani kutoka kazini alivamiwa na watu wasiojulikana na kushambuliwa kiasi cha kuharibiwa jicho, kukatwa kichwa, kung’olewa meno na ukucha.

Hata hivyo akizungumza kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari, Membe alisema ameshangazwa na taarifa hizo na kusisitiza kuwa hahusiki.

“Nimeshangazwa na kusikitishwa na habari hizo, napenda niwahakikishie Watanzania wenzangu kwamba sijahusika, sikuhusika na sina sababu ya kuhusika kwa nanma yoyote ile,” alisema Membe na kuongeza:

“Sina nia, genge wala fedha za kufanya shughuli kama hiyo. Katika maisha yangu yote, sijawahi kugombana naye (Kibanda) na hajawahi kunifanyia ubaya wowote. Kwa kifupi sina uhasama na Kibanda.”

Membe anayetajwa kuwa mmoja wa watakaowania urais mwaka 2015 kupitia CCM, alisema habari hiyo ina malengo ya kisiasa.

“Huu ni mwendelezo wa mkakati wa kisiasa wa kunichafua ambao umekuwa ukiendelezwa na wale wasionitakia mema,” alisema.
Hata hivyo, Waziri Membe ambaye hivi karibuni alisema hatagombea tena ubunge, aliwashukuru watu waliomtumia salamu za kumtia moyo huku akihoji ujasiri wa watu wengine kusema uongo hadharani.

“Jeuri na kiburi cha namna hii hakiwezi kutokana na sheria za nchi, haki ya kikatiba wala hofu ya Mwenyezi Mungu. Naomba Watanzania wenzangu mnisaidie kutegua kitendawili hiki,” alisema Waziri Membe na kuongeza:

“Naamini ukweli kuhusu suala hili utajulikana na yeyote mwenye ushahidi aonyeshe uzalendo wake kwa kutoa taarifa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama.”
Naye Ofisa Mkuu Mtendaji wa New Habari, Hussein Bashe alisema wao wanachotaka ni Waziri Membe ahojiwe kutokana na matamshi yake.

Bashe alidai kuwa, Waziri Membe analalamikiwa kwa mazungumzo yake kwenye kipindi katika kituo cha televisheni moja kudai ana maadui kumi na moja.
“Huyu bwana alitangaza ana maadui kumi na moja na kati ya hao wawili ni waandishi wa habari,” alisema Bashe.

Bashe aliongeza kuwa Waziri Membe alikwenda mbali zaidi na kudai angewashughulikia maadui zake.
“Sasa tayari kuna mwandishi ameumia na yeye (Membe) ana maadui waandishi ndiyo maana tunataka ahojiwe,” alisema Bashe.
Pia, aliongeza kuwa suala hilo lilijadiliwa kwenye kikao cha Wadau wa Vyombo vya Habari hivi karibuni.

 Alisema Waziri Membe anatakiwa kukanusha matamshi hayo siyo suala la kuhusika kumteka Kibanda. Bashe alisema wanaamini vyombo vya dola ndiyo vyenye uwezo wa kumsafisha Waziri Membe, kwa sababu wao wana ushahidi wa kanda wakati anatoa matamshi hayo lakini siyo kwamba wanamhusisha moja kwa moja na tukio hilo la kumdhuru Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate