EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, March 12, 2013

Kigogo wa ajira Polisi matatani afikishwa kwa JK, maofisa wengine watimuliwa

KAMISHNA Msaidizi Mwandamizi wa Polisi aliyekuwa anasimamia ajira katika jeshi hilo nchini, Renatus Chalamila amepewa likizo ya mwezi mmoja baada ya kutajwa mara nyingi kuhusika kuwatoza fedha vijana walioomba ajira za uaskari.

Wakati Chalamila akingoja uamuzi wa rais, maofisa wengine wanne wa jeshi hilo wamesimamishwa kazi na wanatarajia kufunguliwa mashtaka ya kijeshi kutokana na tuhuma mbalimbali za ukiukaji wa maadili na taratibu za jeshi hilo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, akisema kuwa Chalamila amepewa likizo hiyo na mapendekezo kupelekwa kwa rais ili afanye maamuzi juu ya tuhuma zinazomkabili.

Alisema kufuatia hali hiyo, Jeshi la Polisi limelazimika kuwaondoa katika mafunzo askari wanafunzi 95 waliokuwa wamejiunga na chuo cha polisi baada ya kubainika kuwa walipata fursa hiyo kwa kutoa fedha.
Kuhusu tuhuma za maofisa wengine, Waziri Nchimbi aliwataja waliosimamishwa kuwa ni Elias Mwita aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mbeya, msaidizi wake Jacob Kiango na aliyekuwa mkuu wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) wa mkoa huo, Charles Kinyongo.

Alisema kuwa maofisa hao walisimamishwa kazi tangu jana kutokana na kukiuka maadili ya jeshi hilo, wakituhumiwa kupeleka chumvi na sukari kwenye Ofisi ya Mkemia Mkuu badala ya kilo 1.9 ya dawa za kulevya aina ya cocaine zilizokamatwa na askari mkoani Mbeya, Machi mwaka jana.

Kwamba dawa hizo zilikamatwa katika kituo cha Tunduma kisha zikathibitishwa na maofisa wa Mamlaka ya Mapato (TRA) kuwa kweli ni mihadarati.
Waziri Nchimbi alisema vitendo hivyo vinavyofanywa na baadhi ya viongozi wa jeshi vinawavunja moyo na kuwapa hofu askari wa ngazi ya chini ambao hushindwa kufanya kazi zao kwa uadilifu unaotakiwa.

Katika hatua nyingine, aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi mkoani Kagera, Peter Matagi amesimamishwa kazi na atafunguliwa mashtaka ya kijeshi kutokana na kukiuka taratibu za kazi kwa kuwabambikiza kesi zisizo na dhamana wananchi 13 wa Kata ya Nyakasimbi wilayani Karagwe.

Hatua hiyo ni kutokana na vurugu za kugombea ardhi ambazo hazikuwiana na aina ya mashtaka waliyoshtakiwa hali inayoonesha dalili ya uwepo wa rushwa.
Waziri Nchimbi alisema wananchi hao walibambikizwa kesi ya ujambazi wa kutumia silaha ambapo walikaa mahabusu kwa muda wa miezi miwili na baadaye timu ya uchunguzi iliyoongozwa na waziri mwenyewe iligundua kuwa mashtaka waliyoshtakiwa hayakuwa sahihi hali ambayo ilisababisha Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP) afute kesi.

Aliongeza kuwa serikali pia imemsimamisha kazi aliyekuwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Serengeti, Paul Mng’ong’o kwa kosa la kuingia katika hifadhi ya mbuga za wanyama ya Serengeti na kupanga njama ya kuchimba madini aina ya dhahabu hali iliyosababisha kushtakiwa kwenye mahakama ya kiraia.
Waziri Nchimbi alitoa wito kuwa serikali itawaunga mkono askari wanaofanya kazi kwa uadilifu ila watakaoenda kinyume na maadili na taratibu haitasita kuwachukulia hatua za kisheria ikiwemo kuwafukuza kazi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate