EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, March 11, 2013

Ukweli kuhusu masaibu ya Kibanda jicho lake lilipigwa risasi, madaktari waling’oa

WAKATI hali ya Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Absalom Kibanda ikiendelea kuwa tete, ukweli kuhusu afya yake na masaibu yaliyompata umejulikana.

Habari kutoka nchini Afrika Kusini kwenye Hospitali ya Milpark anakotibiwa, zinasema kuwa majeraha aliyoyapata baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana ni makubwa na yatamwacha na ulemavu wa kudumu.

Taarifa kutoka kwa watu walio karibu na Kibanda hospitalini hapo, zinasema kuwa mishipa yote inayozunguka jicho lake la kushoto imevunjika na jicho hilo limesambaratika lote na madaktari sasa, wameamua kuling’oa kabisa.

Madaktari wanne wanaomfanyia uchunguzi na kumpatia tiba Kibanda, wanasema kuwa jicho hilo limesambaratishwa na risasi na atawekewa jicho la bandia ambalo hata hivyo halitaweza kuona.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa awali wa madaktari, kuna madhara kidogo kwenye ubongo wake na kiasi fulani cha damu kimechuruzika kwenye sehemu hiyo ya ubongo.

“Ubongo umedhurika kidogo na madaktari wanampa dawa ya kuyeyusha damu kwenye ubongo. Madaktari wanasema tusiogope, wanaweza kuidhibiti hali hiyo, lakini kipaumbele chao cha kwanza ni jicho. Wakishamaliza jicho ndipo watashughulikia ubongo,” ilisema taarifa hiyo.


Habari zaidi kuhusu afya ya mhariri huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), zinasema kuwa jana alifanyiwa upasuaji kwa saa nne kwa ajili ya kutengeneza upya sura yake, kuweka vizuri paji la uso, na kurekebisha mfumo wa meno.

Pia alifanyiwa upasuaji wa jicho la kushoto na taarifa mbaya ni kwamba madaktari wameshindwa kuliokoa, hivyo wameling’oa.


Taarifa iliyotolewa jana na Katibu wa TEF, Neville Meena, ilisema kuwa madaktari wamechukua hatua ya kitatibu baada ya kuwa tayari jicho hilo lilikuwa limepondeka kwa ndani hivyo lisingeweza tena kuona. Atawekewa jicho la bandia la plastiki ambalo hata hivyo halitakuwa likiona.


“Jambo la kumshuruku Mungu ni kwamba kwa ujumla upasuaji huo uliochukua saa 5 na dakika 30 umefanyika kwa ufanisi mkubwa, na ulikuwa ukiongozwa na madaktari bingwa watatu. Wawili kati yao ni wataalamu wa kichwa na mmoja ni mtaalamu wa macho,” alisema Meena.


Katika upasuaji huo, hakukuwa na madhara ya ndani katika kichwa chake, hivyo kiko salama. Sura yake imejengwa upya kutokana na majeraha ambayo yalikuwa yametapakaa baada ya kupigwa na watu wasiojulikana.


Kwa mujibu wa habari hizo, changamoto kubwa waliyokutana nayo madaktari waliomfanyia upasuaji ni kurejesha katika sehemu yake baadhi ya mifupa midogo inayozunguka jicho, pia kurejesha taya la kushoto ambalo lilikuwa limeathiriwa na tukio la kupigwa kwake. Hata hivyo hatimaye walifanikiwa.

Ripoti kamili kuhusu upasuaji huo inatarajiwa kutolewa leo.


“Tuendelee kumwombea Mwenyekiti wetu Kibanda ili Mungu amponye. Kwa niaba ya Bodi ya Wakurungezi ya Jukwaa la Wahariri, kwa mara nyingine tunampa pole Kibanda pamoja na familia yake na tunamtakia uponyaji wa haraka,” ilisema taarifa hiyo.


Kabla ya upasuaji wa jicho jana, juzi Kibanda alifanyiwa upasuaji kutengeneza upya sura yake, kuweka vizuri paji la uso, na kurekebisha mfumo wa meno.

Upasuaji huo ulifanyika baada ya kupungua kwa majeraha na uvimbe katika sehemu mbalimbali za mwili wake, hususan kichwani na usoni.


Upasuaji huo pia unazingatia matokeo ya uchunguzi uliofanywa kwa zaidi ya saa 48 na jopo la madaktari wanne na kubaini madhara ya awali aliyoyapata mwanahabari huyo nguli.

Kuhusu jicho lake la kushoto ambalo lilijeruhiwa kwa kiasi kikubwa, madaktari walisema wangetoa uamuzi kuhusu aina ya upasuaji ambao wangeufanya baada ya kubaini hali halisi wakati watakapokuwa wakijenga sura yake ambayo iliharibiwa kwa majeraha.


“Wakati akipelekwa kwenye chumba cha upasuaji, Kibanda alikuwa akilalamikia maumivu kutokana na kidonda kilichopo kwenye mguu wake wa kushoto, kidonda hicho pia ni matokeo ya unyama aliyofayiwa,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo ya TEF.

Wakati Kibanda akiendelea na matibabu, jana Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa 

Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana ambao wako Afrika Kusini kikazi, walimtembelea kumjulia hali hospitalini hapo.

Katika salamu zake, Rais Kikwete alisema serikali itawasaka hadi kuwatia nguvuni wahusika wa tukio hilo la utesaji na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.


Jinsi alivyoshambuliwa

Ingawa uchunguzi wa shambulio dhidi ya mhariri huyo umeanza, duru za uchunguzi zinasema kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kundi lililohusika kuwa lile liliomteka, kumtesa na kisha kumtelekeza kwenye Msitu wa Mabwepande, Dk. Steven Ulimboka.

Dk. Ulimboka ambaye ni kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari, aliyeongoza mgomo wa wanataaluma hao, aling’olewa meno, kucha, kupigwa kichwani - staili ya utesaji ambayo pia imetumika kwa Kibanda.


“Ukiangalia jinsi alivyoteswa Kibanda, hakuna tofauti na Ulimboka. Tofauti yake kidogo ni kwamba kwa Kibanda walitumia muda mfupi sana, kama dakika tano hivi. Lakini yote kwa yote, hawa ni watu hatari na ni wataalamu,” alisema mtoa habari wetu kutoka Jeshi la Polisi.

TMF watoa ruzuku kuchunguza

Katika hatua nyingine Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF), umesema utatoa ruzuku ya fedha kuwawezesha waandishi wa habari kufanya habari za uchunguzi kubaini chanzo cha ukatili aliofanyiwa Kibanda.


Mkurugenzi wa TMF, Ernest Sungura katika taarifa yake alisema kuna kila sababu ya kuchunguza tukio hilo ambalo ni mfululizo wa matukio yanayopunguza uhuru wa vyombo vya habari nchini na kuwajengea woga wa kufanya kazi zao.


“Kwa vyovyote vile na kwa sababu zozote, wanaotoa vitisho kwa waandishi na kuwafanyia vitendo vya kikatili ni maadui wa uandishi wa habari za uchunguzi. Ni kwa msingi huu, TMF ipo tayari kutoa ruzuku ya chapuchapu na kuungana na wadau wengine wa habari kuchunguza kilichomtokea Kibanda,” alisisitiza Sungura katika taarifa hiyo.


Alisema TMF katika awamu ijayo, itaandaa mpango mkakati unaolenga kuwalinda waandishi wa habari wanaofanya habari za uchunguzi, ikiwemo kufikiria uwezekano wa kuwawekea bima ya kazi kwenye mazingira hatarishi.

Kibanda alivamiwa na kushambuliwa na watu wasiojulikana nyumbani kwake saa 6.15 usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita, maeneo ya Goba Kunguru, Mbezi Beach, Kata ya Kawe, jijini Dar es Salaam.


Tayari Jeshi la Polisi limeunda tume, huku Jukwaa la Wahariri, nalo limeunda timu maalumu kuchunguza na kubaini waliohusika na tukio hilo.
CHANZO CHA HABARI TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate