EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, March 15, 2013

Wakali wa kike wanaokuja vizuri Nollywood

Ukiachilia mbali mastaa hawa, wako wengine wanaokuja juu kwa sasa ambao watakuja kuchukua nafasi zao kina Omotola kama wao walivyochukua vijiti kwa kina Liz Benson.
Sura hizi mpya sio tu ni vijana bali wana sifa lukuki kama ilivyo kwa mastaa wenzao waliotangulia. 
Kwanza wanavutia na pia wana vipaji. Miongoni mwao wameshinda mataji kadhaa yakiwamo ya urembo na hata uanamitindo.
Je, ungependa kuwafahamu? Hii hapa ni orodha ya waigizaji chipukizi wanaosumbua katika fani ya filamu Nollywood. Licha ya kuwa na msururu mkubwa lakini hawa ndio gumzo kwa sasa;
 
ABUJA, NIGERIA
KAMA ilivyo kwenye soka, katika filamu pia huwa kuna vizazi na vizazi. Kwa kawaida kila kizazi huwa na nyota wake. Na hivi ndivyo ilivyo kwa tasnia ya filamu nchini Nigeria.
 

Wako waliowahi kuwika na kufanikiwa kuliweka juu jina la Nigeria. Miongoni mwao ni pamoja na wakongwe kama vile Patience Ozukwu, Liz Benson, Regina Askia, Clarion Chukwura na Hilda Dokubo
 
Licha ya kuwa juu kwa wakati huo ni ukweli usiopingika kuwa bado wanaendelea kufanya vizuri kwa sasa.
Katika kizazi kilichopo wapo mastaa wa kike ambao wanatamba zaidi. Unapoweka orodha ya mastaa hao huwezi kukosa watu kama Omotola, Genevieve, Mercy Johnson, Chika Ika, Stella Damasus, Ini Edo na Tonto Dike.
 
Damilola Adegbite
Damilola Adegbite hana muda mrefu kwenye filamu. Lakini kwa jinsi anavyofanya kazi kwa bidii anakubalika na wapenzi wengi wa filamu za Kinigeria.
Hivi sasa anakuja na filamu yake mpya iliyotengenezwa na prodyuza, Michelle Bello itakayofahamika kwa jina la Flower Girl.

Kwa jinsi alivyoitendea haki filamu hiyo hutasita kumuita Flower. Licha ya filamu hiyo, mrembo huyu aliwahi kutokea kwenye tamthilia moja maarufu nchini Nigeria inayofahamika kwa jina la Tinsel akiigiza kama Thelma Duke. Hapo ndipo alipoamua kutoka huko na kujikita kwenye filamu.
Lilian Esoro
 
Naye alianzia kwenye tamthilia. Aliwahi kufanya tamthilia ya Clinic Matters akiigiza kama Nurse Abigail
 
Kutokana na juhudi aliyokuwa nayo katika suala zima la uigizaji, hivi karibuni ameungana na wakali Mercy Johnson na Funke Akindele kwenye kinyanganyiro cha tuzo za Africa Magic Viewers Choice (AMVCA), yumo katika kipengele cha Mwigizaji Bora wa kike katika kifungu cha uchekeshaji.
Beverly Naya
 
Ni miongoni mwa warembo wenye kujiamini. Hii ni kutokana uwezo alionao katika suala zima la uigizaji. Mwaka jana aliingia katika kinyanganyiro cha kuwania nafasi ya mwigizaji bora katika mitindo kupitia jarida la FAB nafasi ambayo ilienda kwa Rita Dominic baada ya kuwabwaga waigizaji wengine kama Genevieve Nnaji, Omotola Jalade na Nse Itse-Akpan.
 
Ukiachilia mbali kushiriki mrembo huyu ameshawahi kushinda tuzo kadhaa. Miongoni mwa tuzo ni pamoja na ile ya Kipaji Chipukizi Bora kwa mwaka 2010. Ilikuwa kwenye tuzo za ubora za Nollwood, pia mwaka 2011 aliwahi kushinda tuzo ya Msanii anayekuwa kwa kasi.
Biola Ige
 
Biola Ige sio mgeni sana kwenye fani ya uigizaji. Ispokuwa kutokana na kuzongwa na shughuli za utafutaji maisha alitoka kidogo. Lakini kwa sasa amerudi tena katika tasnia ya uigizaji.
 
Wapenzi wa filamu wanamtaja kuwa ni miongoni mwa waigizaji wenye macho mazuri katika Nollywood, si hivyo tu anatajwa pia kuwa mwenye umbo la kuvutia.
Katika kipindi cha miaka minne alichodumu kwenye tasnia ya uigizaji, ameripotiwa kuigiza filamu 20.

Collete Orji
Collete ameingia kwenye tasnia ya uigizaji muda mfupi uliopita. Lakini kutokana na umahiri wake katika uigizaji, tayari ameweza kukubalika hata kwa watengenezaji filamu mbalimbali.
Ni miongoni mwa warembo waliojaaliwa uzuri , kipaji na hata umbo la kuvutia. Kutokana na sifa zake hizo ameweza kupata nafasi katika filamu kadhaa zikiwamoStrength of a Woman, Blue Blood, Raindrop na Two Can Play That Game.

Angel Ufuoma
Kitaaluma Angel Ufuoma ni Mwanasheria. Lakini baada ya kugundua ana kipaji cha ziada ambacho ni uigizaji hakusita kujiingiza huko.
Amekuwa kwenye fani ya filamu kwa muda wa miaka mitatu sasa. Lakini amekuwa akiigiza kwa umahiri mkubwa sana kiasi cha kukubaliwa na wengi.

Chelsea Eze
Sifa yake ya kushinda tuzo kadhaa za vipaji, ilitosha kumweka juu kwenye tasnia ya filamu na hata kuwa miongoni mwa waigizaji wa kike wanaokuja juu kwa sasa.
Namzungumzia mrembo aliyeigiza katika filamu za Two Brides And A Baby, Twist,Timeless Passions na Hood Rush.
Kutokana na umahiri wake, waongozaji na hatawaigizaji wakubwa wamekuwa wakimkubali na hivyo kuigiza naye kwa kuwa mwigizaji msaidizi na hata mwigizaji mkuu. Kujituma kwake ndio siri ya mafanikio yake.

Tope Osoba
Kama ilivyo kwa waigizaji kama Omotola Jelade au Mercy Johnson, mwigizaji huyu ana uwezo mkubwa wa kushika nafasi mbalimbali tena, yaani uhusika wowote.
Katika kudhihirisha hilo hakusita kufanya maajabu katika filamu za Gucci Girls, Omo Tee, Oogun Mi, 21 Million.
Urembo na kipaji alichonacho vimekuwa vikimwongezea mapenzi dhidi ya mashabiki wake na hivyo kuzidi kuonekana tishio katika tasnia ya uigizaji.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate