EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, March 15, 2013

Raha ya mapenzi ni furaha

HAKUNA ubishi kwamba maisha ukiyapangilia ni mazuri sana, yatakupa amani na kwa ujumla utatamani uendelee kuishi milele, usipokuwa makini utaishia kujuta.
 
Uamuzi wako ndio hutengenezahatma ya maisha yako; je unavyoamua ni sahihi? Kila mtu analo jibu. Ikiwa tayari uko kwenye uhusiano, na unamkubalia mwanamume mwingine kwa sababu zozote, ni dalili kwamba akili yako imekufa.

Katika maisha kuna watu wamekuwa wakilia kwa raha, wengine kwa taabu, wengine wamekuwa wakicheka bila hata kuchekeshwa mara nyingi ni kwa sababu wanatiwa raha. Je, mara ya mwisho kufurahi au kukaa na mwenzi wako na mkafurahi ni lini?

Jambo ambalo unapaswa kubaki nalo kupitia makala haya ni kwamba watu wanaingia kwenye uhusiano kwa ajili ya kusaka raha, sio kusaka watu wa kuwapiga makofi, si kusaka watu wa kuwatukana na kuwakosesha amani.

Hii ina maana kwamba kama uko kwenye uhusiano, fanya uwezalo kuhakikisha unamtia raha mwenzi wako. Kama hapati raha, ni suala la kukaa na kuangalia nini cha kufanya ili mwenzi wako aweze kuwa mwenye raha. Duniani tunapita, yanini kutendeana mabaya jamani?

Inasikitisha kwamba kuna watu wamekuwa wakianzisha uhusiano kwa raha, wanafanyiana mazuri mengi, wanapanga mikakati mingi mizuri, lakini inafikia wakati watu hao hao wanaanza kutiana shida, kutukanana, kupigana na kunyanyasana kwa namna moja ama nyingine.

TOFAUTI YA ELIMU, KIPATO
Hilo swali nimekuwa nikiulizwa na wasomaji wengi mno, huwa sipendi kulizungumzia.

Ukweli ni kwamba ndoa nzuri au mbaya inategemea na malezi au tabia ya mtu kwa ujumla. Ndoa nyingi ambazo mmoja yuko juu sana na mwingine yuko chini sana, mara nyingi huwa ni ya maigizo.

Nje wanaonekana wana ndoa, ndani ni shida. Binafsi sijaweza kufanikiwa kushuhudia ndoa nyingi za wanawake matajiri sana au wenye majina makubwa ambazo ndani zina amani sana, labda kama watakuwa imara katika dini.

Kwa hiyo kama unafikiria kuoana na mwanamke imara sana kiuchumi, au kielimu, sikushauri uache au uendelee, uamuzi ni yako, ila jitahidi kuhoji ni kwanini hajaolewahasa kama ana umri wa miaka 35 na kuendelea.

Najua atakueleza sababu nyingi kwanini aliachana na fulani, ambazo nyingi zitakuwa ni za kuonyesha alioachana nao ndio walikuwa wabaya, ndivyo wengi wanavyofanya.

Tafakari kwa makini zaidi, hasa kama alishawahi kuwa na mtoto au watoto au kuwapo kwenye ndoa na kutalakiana.Kuwa kwenye ndoa ni kuzuri, ni hatari zaidi kama unakuwa kwenye ndoa na mtu ambaye hakupi amani, kwani kitaalam utakufa haraka kwa kupata magonjwa kama ya moyo nk.Heri kuishi mpweke kuliko kuwa kwenye uhusiano usiokupa amani.

TAFAKARI SANA; Kama unaanzisha na mtu ambaye tayari alishakuwa kwenye ndoa, uwe makini mno. Lakini uwe makini zaidi kama mtu huyo naye wazazi wake wametalakiana, uwezekano wa ndoa yenu kutofika mbali ni mkubwa, kwa sababu katika fikra za mtu huyo huwa wanapata majibu ya haraka achana na mimi bwana mbona hata baba aliachana na mama na aliishi.

KWA WANAOTAKA KUANZISHA UHUSIANO; Pata muda wa kumchunguza vizuri mwenzi wako kabla ya kuamua awe mke au mumeo. Pia ni vizuri kutofanya ngono, kwa sababu hilo tendo ndilo linalosababisha wanawake wengi wanaishia kudanganywa.eeeh unakuta mtu hamjakubaliana kuoana halafu mko kwenye tendo unamuuliza unajisikiaje.eeeeh kwa hiyo utanioa? Haaa ha ha!! Nafikiri unachotafutwa hapa ni kudanganywa.

Utakachojibiwa ni kwamba Unataka ndoa, haina shida nitakuoa, hata kesho.eeeh ni kwa sababu jamaa wakati huo akili yake inakuwa haiko hapo, kinachoongea ni mdomo, lakini yeye hayuko. Kwa hiyo ndugu zangu wadada, lazima uangalie unaongea naye mtu wakati gani.

ZAWADI GANI NZURI KWA MWENZI WAKO?; Kuna baadhi ya wasomaji wameuliza je ni zawadi gani nzuri ya kumpa mwenzi wako?

Hili swali naona kama tunateganamaana ukweli watu siku hizi wanapenda fedha zaidisawa unaweza kumpelekea ua, unaweza kununua nguo nk, lakini watu wanapenda fedha.

Zawadi ifaayo katika maisha ya ndoa ni kupendana kwa dhati na kufanyiana mambo mazuri. Mheshimu mwenzi wako, na endelea kubuni mambo mazuri ya kumfanyia. Kama kweli unampenda, ni wazi hutapenda awe mnyonge. Katika mapenzi kila mwanandoa anapaswa kufahamu kuwa analo deni la kumpenda na kumfanyia mema mwanandoa mwenzake.
MADA NA DISMAS LYASSA WA MWANASPOT

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate