MTANGAZAJI
wa Kituo cha Redio cha Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ amewashangaza
watu baada ya kutundika mtandaoni picha zinazomuonesha akioga bafuni
huku nyingine akiwa maliwatoni.
Picha
hizo zinapatikana kwenye mtandao wake na hakueleza ilikuwa wapi ila
akasema ilikuwa ni siku alipoamua kuitumia wikiendi yake ipasavyo katika
hoteli ambayo hakuitaja jina.
Baadhi ya watu waliyoziona picha hizo walimponda wakidai eti ni ulimbukeni lakini wapo waliomtetea kwa kusema, ni staili tu ya maisha aliyoamua kuishi.
“Ushamba
tu, ndo nini sasa? Angetuwekea ‘akikata gogo’ pia,” alisema mmoja wa
wadau huku mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Dick akisema:
“Msimuonee wivu mwenzenu, anakula bata zake na nyie hamjakatazwa.”
Dida alipoulizwa kuhusu kujianika hivyo alisema, hizo ni ishu zake binafsi na wapenzi wake wanapenda kuona kila anachokifanya, ndiyo maana anawawekea kwenye blogu yake.
Baadhi ya watu waliyoziona picha hizo walimponda wakidai eti ni ulimbukeni lakini wapo waliomtetea kwa kusema, ni staili tu ya maisha aliyoamua kuishi.
Dida alipoulizwa kuhusu kujianika hivyo alisema, hizo ni ishu zake binafsi na wapenzi wake wanapenda kuona kila anachokifanya, ndiyo maana anawawekea kwenye blogu yake.
No comments:
Post a Comment