EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 4, 2013

M2 THE P ANA USHAHIDI WOTE KATIKA KIFO CHA ALBERT MANGWEA.

Na Mwandishi Wetu
MBIVU na mbichi sasa zinaweza kujulikana, kinachoombwa ni muda tu, kwani mng’amuzi halisi kuhusu kifo tata cha mwanamuziki mwenye kipaji kikubwa Bongo, Albert Mangwea ‘Ngwea’, yupo kwenye mazingira mazuri kueleza kilichotokea.

KWA NINI ANA USHAHIDI WOTE?
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Mgaza Pembe ‘M2 The P’, ndiye mwenye ushahidi wote kwani aliambatana na Ngwea kila sehemu waliyotembelea mpaka nukta ya mwisho nchini Afrika Kusini.
M2 The P, alipatwa na matatizo sawa na marehemu Ngwea, isipokuwa mwenzake ilifikia hatua mbaya na kupoteza maisha huku yeye akibaki mahututi kwenye chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) katika Hospitali ya St. Helen Joseph, jijini Johannesburg nchini humo.
Jambo la faraja ni kwamba, M2 The P yupo vizuri kwa sasa, atakaporuhusiwa kutoka, atajibu maswali mengi tata ambayo yamejitokeza tangu Ngwea alipofariki dunia Juni 28, mwaka huu, nchini humo  alipokwenda kwenye shughuli zake.

JAWABU LA SUMU 
Moja ya mambo yanayozungumzwa pembeni ni kwamba kuna uwezekano mkubwa marehemu Ngwea na M2 The P  waliwekewa sumu kwenye chakula au kupuliziwa ‘laivu’ kisha kutokea yaliyotokea, lengo likiwa kuwadhulumu mzigo wa fedha nyingi waliokuwa nao, hivyo kupona kwa mmoja huyo ni matakwa ya Mungu ili awe shahidi namba moja wa kifo cha Ngwea.
“Ni jambo la kumshukuru Mungu jamani, M2 The P anaendelea vizuri sana, kwa sasa anazungumza. Naamini yeye amepona kwa ajili ya kufichua kilichofichika nyuma ya kifo cha mwenzake.
“Kama kweli walilishwa sumu kwenye chakula au walipuliziwa au lolote lile lingine, M2 The P anajua kila kitu kwani walikuwa wote kwa siku nzima mpaka wanarudi nyumbani alfajiri kwa safari ya kurudi Bongo.

“Awali tuliposikia M2 The P naye amefariki dunia sisi Wabongo wa huku tuliumia sana, tukasema sasa nani atafichua kilichotokea? Lakini Mungu mkubwa,” alisema Tony, Mbongo anayeishi Sauzi akifanya biashara halali.

HOFU YA KUUAWA M2 THE P
Baadhi ya watu waliishauri Serikali ya Tanzania kufanya kila liwezekanalo, M2 The P alirudi Bongo wakidai kama kweli wawili hao walilishwa sumu kwa namna yoyote ile, wahusika watafanya juu chini kuuondoa uhai wake ili kupoteza ushahidi.
Walisema kama ni sumu, wahusika watakuwa bado wapo ndani ya nchi hiyo na kwa vile M2 The P hana ndugu wa damu kule, si rahisi kulindwa kwa kiwango cha kutambua nani mbaya kwake.

MADAI YA UNGA KWA M2 THE P
Kumekuwa na madai kwamba, Ngwea alifariki dunia kwa ‘kujiovadozi unga’ lakini kama kweli msanii huyo alikuwa akitumia ‘mambo’, madai hayo yanapingana na ukweli kuhusu M2 The P kwamba si mtumiaji wa unga.
Kwa maana hiyo kama M2 The P si mtumia unga kwa nini na yeye alikumbwa na dhahama ileile iliyomkumba mwenzake? Kuna zaidi ya kitu hapo.
Juzi, Uwazi liliwatafuta baadhi ya wasanii wa Bongo Fleva waliowahi kufanya kazi karibu na M2 The P na kuwauliza kama wanajua chochote kuhusu madai ya msanii huyo kubwia unga kama Ngwea, wote walikanusha.
“Jamaa (M2 The P) hatumii unga, we si unaona hata afya yake? Mtu anayetumia unga anajulikana hata kwa macho kaka,” alisema Mbongo Fleva mmoja mwenye jina kubwa Bongo akitokea upande wa Temeke.
Ndugu mmoja wa karibu na msanii huyo alipopigiwa simu na kuulizwa kuhusu madai hayo, alisema aliwahi kusikia tetesi hizo mwaka jana, alipofanya uchunguzi alishindwa kupata ukweli huku mtuhumiwa mwenyewe akikataa katakata kubwia madawa ya kulevya.

DALILI  ZA MBWIA UNGA
Kwa mujibu wa kitaalam, binadamu anayetumia unga hupoteza nguvu na uwezo wa kufanya mambo aliyokuwa akimudu kuyafanya awali.
Akizungumza na Uwazi juzi, daktari wa zahanati moja iliyopo Kimara, Dar es Salaam (jina tunalo)  alitoa mfano wa kitaalam kwamba, mcheza mpira anayemudu kukaa uwanjani kwa dakika 90 anapotumbukia kwenye matumizi ya madawa ya kulevya hupoteza uwezo huo na pengine kumudu kuwepo kwa dakika 45 tu.
Alisema unga una tabia ya kummaliza nguvu mtumiaji, hasa asiye na uwezo wa kupata lishe nzuri hivyo kupoteza uwezo mkubwa wa awali, jambo linaloweza kuwafanya wengine kuona mabadiliko hayo ya wazi.
“Kuna mchezaji wa timu moja kubwa nchini, awali alikuwa akisifika kwa kucheza mpira vizuri, tena kwa muda wote, alipoanza kutumia unga uwezo wake uwanjani ulishuka kabisa na ikafika hatua akawa hapangwi hadi kiongozi mmoja wa timu alipombaini,” alisema dokta huyo.

M2 THE P ALICHEZA MPIRA KWA DAKIKA 90
Julai 7, 2012 kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini linalofanyika Uwanja wa Taifa, Dar kila mwaka (hata mwaka huu lipo), M2 The P alichezea Timu ya Bongo Fleva inayowashirikisha wasanii wa muziki wa kizazi kipya.
Msanii huyo alimudu kucheza mpira kwa dakika zote 90, hali inayoweza kuondoa wasiwasi kwamba ni mtumiaji wa unga kama inavyodaiwa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate