EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 15, 2013

Chadema yaitesa CCM uchaguzi wa udiwani Arusha

Arusha. 
Chadema kimethibitisha umwamba wake katika siasa za Jimbo la Arusha Mjini, baada ya kutetea kwa kishindo kata zake nne kwenye uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika jana.

 
Katika uchaguzi huo uliokuwa unasubiriwa kwa hamu na ambao ulichukuliwa kama kipimo cha siasa za Arusha ambazo zimekuwa na mvutano mkubwa, Chadema kiliongoza katikia vituo vyote 136 vya kupigia kura Kata za Elerai, Kaloleni, Kimandolu na Themi.

Kata hizo zilikuwa wazi tangu mwaka 2011 baada ya Chadema kuwatimua wanachama wake waliokuwa madiwani Estomih Mallah(Kimandolu), John Bayo (Elerai), Reuben Ngowi (Themi) na Charles Mpanda (Kaloleni).


Matokeo

Katika matokeo yaliyotangazwa na Msimamizi wa Uchaguzi Kata ya Elerai, Obedi Meng’oriki mshindi alikuwa Jeremiah Mpinga wa Chadema aliyepata kura 2,047 dhidi ya 1,471 za Emmanuel Laizer wa CCM. Katika Kata hiyo kulikuwa na wagombea wengine ambao ni John Bayo (CUF; kura 302), Seif Shimba (CCK; kura 3) na Boisafi Shirima (TLP;1).


Katika Kata ya Themi, Kinabo Edmund wa Chadema aliibuka na ushindi baada ya kupata kura kupata kura 674. Msimamizi wa Uchaguzi Kata hiyo, Ezeka Mboya alisema Kinabo alifuatiwa na Victor Mkolwe aliyepata kura 326 na Lobora Ndarpoi wa CUF alipata kura 307.


Kata ya Kaloleni, Msimamizi wa Uchaguzi, Anna Ledisa alimtangaza Kessi Lewi wa Chadema kuwa mshindi kwa kura 1,470 dhidi ya Emmanuel Mliari wa CCM aliyepata kura 330 na Abbas Mkindi wa CUF aliyepata kura 275 na Ngilishi Pauli wa Demokrasia Makini aliyeambulia kura mbili.


Kata ya Kimandolu, Msimamizi wa Uchaguzi, Suleiman Kilingo alimtangaza Mchungaji Rayson Ngowi wa Chadema kuwa mshindi kwa kura 2,761 na kumshinda Edna Saul wa CCM aliyepata kura 1,163. Kwa matokeo hayo, Chadema sasa kimefikisha madiwani 12 wakati CCM kimebakiwa na kumi na moja na TLP kina wawili.


Ushindi huo wa Chadema una athari kwa nafasi ya Meya wa Jiji la Arusha, Gaudence Lyimo kwani CCM kina wajumbe 14 tu kwenye Baraza la Madiwani, TLP wawili wakati Chadema sasa kimefikisha 15. Wabunge wa majimbo na wale wa viti maalumu pia ni madiwani.



Aidha, Chadema kina nafasi ya kuongeza kiti kingine cha udiwani kwani Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kinatarajiwa kuitisha uchaguzi mdogo Kata ya Sombetini.


Mkurugenzi wa NEC, Julius Malaba alimwambia mwandishi wetu kuwa tume yake inatarajia kuitisha uchaguzi mdogo hivi karibuni baada ya kata hiyo kutangazwa wazi na 
Ofisi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tamisemi.

Malaba alisema uchaguzi huo utaitishwa baada ya aliyekuwa Diwani wake, Alphonce 

Mawazo kujitoa CCM na kujiunga na Chadema hali inayokifanya chama tawala kuwa katika wakati mgumu kukitetea kiti hicho.
 
Wachache wajitokeza
Uchaguzi ulikuwa na idadi ndogo ya wapigakura kulinganisha na chaguzi zilizopita.
Elerai inayoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wapigakura 23,885 waliojitokeza ni 3,824 tu ikifuatiwa na Kimandolu yenye wapigakura 17,209 lakini waliopiga kura ni 3,967.
Kata ya Kaloleni ina wapigakura 12,674 hata hivyo, waliopiga kura ni 2,292. Themi yenye wapigakura wachache kuliko zote ikiwa na watu 6,387 lakini waliojitokeza kupiga kura ni 1,319 tu.

Licha ya idadi hiyo ndogo, baadhi ya wapigakura waliojitokeza walishindwa kutimiza dhamira yao baada ya kugundulika dosari kadhaa kwenye vitambulisho vyao na Daftari la Kudumu la Wapigakura.

“NEC wamevuruga uchaguzi huu makusudi kwa kuchezea Daftari la Wapigakura kwa nia ya kukibeba CCM. Haiwezekani waliopiga kura Uchaguzi Mkuu mwaka 2010 leo hii waambiwe majina yao hayamo kwenye daftari,” alilalamika mgombea udiwani Kata ya Kaloleni, Abbas Mkindi ‘Darweshi’.

Mkindi aliyewania kiti hicho kupitia CUF alitoa mfano wa mtoto wake, Omar Othman mwenye kitambulisho cha mpigakura namba 32479962 alichokitumia mwaka 2010 kuzuiwa kupiga kura baada ya jina lake kukosekana kwenye Daftari hilo. Wapiga kura wengine, Godchan Msella mwenye kadi namba 32479396  na Richard Minja mwenye namba 32479311 alizuiwa kupiga kura baada ya kubainika kuwa namba iliyopo kwenye Daftari ni tofauti na ya kadi yake.

Kutokana na kuwapo kwa mkanganyiko huo, Makamu Mwenyekiti wa NEC, Hamid Mohamoud Hamid alilazimika kuwaita wataalamu wa mfumo wa kompyuta (IT), katika Kituo cha Kupiga Kura cha Kaloleni kusaidia, kazi ambayo ilifanywa na timu iliyoongozwa na Seif Mtero.

Malaba alikiri uwezekano wa kutokea tofauti za tarakimu kwenye vitambulisho vya wapigakura na Daftari la Kudumu la Wapigakura huku akishauri wasimamizi na mawakala wa vyama kutumia busara kuruhusu wananchi wenye vitambulisho na maelezo sahihi kupiga kura.

“Tofauti ya tarakimu kwenye kadi ya mpigakura na Daftari la Mpiga Kura ni kosa la NEC, hivyo siyo sahihi kuwahukumu wapiga kura kwa kuwanyima haki yao ya kuchagua viongozi wawapendao,” alisema Malaba.

Amani yatawala
Ukiacha dosari na idadi ndogo ya wapiga kura, uchaguzi huo ulifanyika kwa amani na utulivu mkubwa tofauti na hofu iliyokuwapo awali kwamba huenda vurugu zingeibuka kutokana na mvutano uliopo kati ya vyama vya CCM na Chadema.

Hata hivyo, kulikuwa na kamatakamata na baadhi ya waliotiwa mbaroni ni wale waliokutwa na vitambulisho feki vya kupiga kura.

Katika eneo la Shule za Msingi Kimandolu na Elerai, watu wawili walikamatwa kwa kukutwa na shahada feki za kura. Kimandolu msichana aliyejitambulisha kwa jina la Mariamu alikamatwa baada ya kwenda na kadi inayodaiwa kuwa feki.

Mpiga kura huyo alikamatwa na msimamizi wa uchaguzi ambaye ni Mtendaji wa Kata hiyo, Selemani Kikingo na kukabidhiwa kwa polisi.

Katika Kata ya Elerai, Zainabu Mohamed pia alikamatwa kwa tuhuma za kuwa na shahada yenye utata na baadaye kukabidhiwa polisi.

Katika maeneo hayo, pia vijana ambao waliokataa kuondoka karibu na vituo baada ya kupiga kura walikamatwa.
Credit; Mwananchi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate