EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 16, 2013

Meya CCM akalia kuti kavu Arusha

Arusha. 
Kitendo cha Chadema kutetea viti vyake vinne vya udiwani kwenye uchaguzi mdogo wa juzi, kimetafsiriwa kwamba ni kumfanya Meya wa Jiji la Arusha, Gaudence Lyimo kukalia kuti kavu. Kwa ushindi wake huo, Chadema kimefikisha viti 15 kwenye Baraza la Madiwani la Arusha wakati CCM kimebakiwa kuwa na viti 12 wakati TLP ina viti sita.
 
Pia Chadema kina nafasi ya kuongeza kiti zaidi kwani ina nafasi moja ya viti maalum iliyokuwa ikishikiliwa na Rehema Mohamed aliyetimuliwa mwaka 2011.

Mwenyekiti wa madiwani wa Chadema, Isaya Doita alisema jana kwamba ushindi wa juzi ni chachu katika msimamo wa chama chao kutaka uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha urudiwe akiamini kuwa alichaguliwa kimizengwe.

Doita ambaye ni Diwani wa Ngarenaro, alisema wana imani muda si mrefu Jiji la Arusha sasa litapata Meya ambaye amechaguliwa kwa misingi ya sheria.

Chadema ilitetea viti vya Kata za Themi, Kimandolu, Kaloleni na Elerai ilivyovipoteza baada ya kuwafukuza waliokuwa madiwani wake kwa kosa la kukiuka maagizo ya Kamati Kuu ya chama hicho kuhusu mwafaka wa umeya.

Ushindi huo unakihakikishia wingi wa wajumbe katika baraza hilo la madiwani hivyo kuwa na fursa kumwondoa madarakani Meya Lyimo. Doita aliahidi kuwa chama hicho kitakaa leo kutoa msimamo kuhusu suala hilo la umeya wa Arusha.

Akizungumzia suala hilo, Katibu wa CCM wa Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda alisema Chadema kisahau suala la kuchagua meya mpya kwani uchaguzi wake ulishapita.
Chatanda, ambaye pia anaingia katika vikao vya Baraza la Madiwani la Arusha kutokana na kuwa Mbunge wa Viti Maalumu, alisema Chadema kinapaswa kufanya kazi na meya wa sasa.

“Unajua vikao hivi vinaongozwa kwa kanuni, kwa hiyo wingi wao si hoja ya kumvua meya au kulazimisha kupitisha mambo yao,” alisema

Mamia wafurika Manispaa
Wabunge wanne wa Chadema jana waliongoza mamia ya wafuasi wa chama hicho katika shamrashamra ya kuwasindikiza madiwani wanne kwenda kujitambulisha kwa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha.

Hata hivyo, furaha yao ilizimwa na polisi baada ya kumuomba Mbunge Arusha Mjini, Godbless Lema kuwatawanya.


Wabunge wengine walikuwa Mchungaji Israel Natse (Karatu), Joshua Nassari (Arumeru Mashariki) na Grace Mukya (Viti Maalumu) ambao walitokea ofisi za Chadema Mkoa wakiwa na wafuasi wa Chadema wakiwamo vijana wa bodaboda, magari na watembea kwa miguu.

Wakati wabunge hao, wakiwa katika magari yao, Madiwani wanne wa Chadema, walioshinda, Mchungaji Rayson Ngowi (Kimandolu) Edmund Kinabo(Themi), Mhandisi Jeremiah Mpinga (Elerai) na Kessy Lewi (Kaloleni), walikuwa katika gari la wazi.

Hata hivyo, walipofika katika eneo la Halmashauri waliwakuta polisi wakiwa wametanda katika eneo hilo na kuwaruhusu wabunge, madiwani na viongozi pekee kuingia. Agizo la Kamanda wa Polisi Wilaya ya Arusha (OCD), Gillis Mrotto kuwataka wafuasi hao kutawanyika halikufanikiwa hadi alipomuomba Lema kuwatawanya wafuasi hao.

Akizungumza na madiwani hao, Mkurugenzi Jiji, Sipora Liana aliwaahidi ushirikiano: “Nawapongeza na naomba tushirikiane katika kazi. Mimi kwa kawaida sipendi ubadhirifu.”

Mbowe ajisalimisha Polisi
Jeshi la Polisi Makao Makuu limemhoji Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kwa madai kuwa kauli zake alizozitoa baada ya kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho ni za uchochezi.

Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi  ya Upinzani Bungeni alihojiwa kutokana na madai kwamba alisema polisi ndiyo waliohusika na ulipuaji wa bomu Arusha, waliisaidia CCM kwenye uchaguzi na kumtuhumu Rais Jakaya Kikwete kuhusika na mauaji ya Arusha kutokana na kukaa kwake kimya.

CREDIT: GAZETI LA MWANANCHI.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate