EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, July 11, 2013

Tunamshangaa Spika Makinda kuwa Kambi ya Upinzani Bungeni, imekuwa ikiwahonga waandishi wa habari.

Habari na GAZETI LA MTANZANIA
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda, ameibua mjadala ambao tunaona hauwezi kupita hivi hivi bila kuujadili. Spika Makinda amekuwa mmoja wa viongozi wakubwa wa taifa hili, ambao kila kukicha wanaibua mijadala mingine ambayo haina tija hata kidogo kulingana na wadhifa wake.
Juzi, Spika Makinda ameibua mjadala ambao alidai kuwa waandishi wa habari wamekuwa wakihongwa na Kambi ya Upinzani Bungeni, ili waandike habari zao kwa wingi, kuliko wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kwa maneno yake bila haya, Spika Makinda anasema waandishi wamekuwa wakipewa ‘kitu kidogo’ (rushwa) katika mikutano ya Bunge inapofanyika mjini Dodoma.

Tumeshangazwa mno na Spika Makinda kutoa maneno haya, ambayo tunaamini akibanwa vizuri atoe ushahidi atabaki mdomo wazi.

Kwa kipindi kirefu tangu akabidhiwe kiti hicho, Spika Makinda amekuwa kiongozi mwenye kauli za kusikitisha mara nyingi na kutuhumiwa kukalia hoja nzito nzito zinazoelekezwa serikalini.

Pia amekuwa akilalamikiwa mno kuwakandamiza wabunge wa upinzani na hata wananchi wa kawaida tu wamekuwa wakijiuliza namna Spika Makinda anavyoendesha mhimili huo.

Hakuna ubishi kwa nyakati tofauti, Spika Makinda amekuwa akilalamikiwa kuwapendelea zaidi wabunge wa CCM katika mambo mengi.

Lakini si nia yetu kueleza mambo mengi, lakini tunataka Spika aueleze umma ni namna gani anavyopotosha jamii juu ya mhimili wa vyombo vya habari.
 
Tunamtaka ajitokeze hadharani na atoe ushahidi hadharani ambao unaonyesha Kambi ya Upinzani Bungeni, imekuwa ikiwahonga waandishi wa habari.

Sisi MTANZANIA, tunamtaka Spika Makinda ajitokeze hadharani na kuviomba radhi, kwani asipofanya hivyo, atakuwa amejipaka matope.

Tunasisitiza kama hatafanya hivyo, ipo siku atajikuta waandishi wanaweka chini kalamu zao na kuacha kuandika habari muhimu za Bunge ambazo wananchi wanapaswa kuzipata wakati wa vikao vya Bunge.

Tunamalizia kwa kuhoji, hivi Spika Makinda hana washauri katika mambo ya msingi na yenye maslahi kwa taifa? Ndiyo maana tunasema tunamshangaa Spika Makinda.

                           
                       CHANZO CHA HABARI NI GAZETI LA MTANZANIA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate