EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, September 3, 2013

Miswada ya Katiba ‘kulipua’ Bunge kesho

Dodoma.
Miswada ya Sheria ya Marekebisho ya Mabadiliko ya Katiba na wa Kura ya Maoni inayotarajiwa kuanza kuwasilishwa bungeni kesho inaonekana kuwa kaa la moto kwa Serikali kutokana na wabunge wengi kujipanga kupinga baadhi ya vifungu.

Vyanzo mbalimbali viliwaambia waandishi wetu jana kuwa kumekuwapo na mvutano mkali miongoni mwa wajumbe wa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala ya Bunge kiasi cha kuilazimisha Serikali kukubali baadhi ya mapendekezo muhimu.
 
Habari zimeeleza kuwa kutokana na mvutano huo, wiki iliyopita wajumbe wa kamati hiyo walirudisha miswada hiyo kwa Serikali ili kuifanyia marekebisho na kuirudisha tena mbele ya kamati.

“Hata sasa hivi tunapozungumza (jana mchana), kamati inakutana ili kupitia tena vipengele vya miswada hiyo,” kilidokeza chanzo chetu bila kufafanua kama ilikuwa inajadili vipengele vipya au la.

Hata hivyo, Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, William Ngeleja alisema hakukuwa na mvutano wowote kati ya kamati yake na Serikali bali, majadiliano ya kawaida tu ili kuweka mambo sawa.


“Unajua kwenye maandalizi ya miswada mara nyingi kunakuwapo mashauriano mengi kati ya Serikali na kamati husika,” alisema Mbunge huyo wa Sengerema (CCM).
Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe alikiri kupokea mapendekezo kutoka kwa wabunge na hasa kwenye Sheria ya Marekebisho ya Mabadiliko ya Katiba akisema wametaka kuangaliwa upya kwa kipengele cha Kamati ya Uteuzi ya viongozi wa Bunge la Katiba. Alisema sasa wataweka sifa za mwombaji wa nafasi hizo na wasiokuwa nazo hawatagombea.

Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa alisema moja ya mambo ambayo yanabishaniwa ni hatua ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kupewa mamlaka ya kusimamia kura ya maoni wakati taasisi hiyo inalalamikiwa kwa kutokuwa huru.
Alisema kipengele kingine ni siku 30 zinazopendekezwa na sheria za kufanya kampeni kwa wananchi kwa ajili ya kupiga kura ya Ndio au Hapana akisema ni muda mdogo mno.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali, moja ya mambo yanayopingwa na wabunge ni ile sheria ya kuwapata wajumbe wa Bunge la Katiba hilo kutoka katika makundi ya jamii.
Muswada wa Katiba ya Mabadiliko ya Katiba unataka wawakilishi kutoka makundi ya Jamii kuwa 166 katika Bunge la Katiba lakini wabunge wanataka idadi iwe 200.

Mbunge wa Muhambwe, Felix Mkosamali (NCCR-Mageuzi) alisema uzoefu katika nchi nyingine unaonyesha Mabunge ya Katiba hushirikisha watu wengi ili kupata uwakilishi mpana tofauti na mapendekezo ya miswada hiyo.

Mkosamali ambaye pia ni mjumbe katika Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, alisema ni vyema sheria ikasema wajumbe wa Bunge hilo watatoka katika taasisi zipi.

Kifungu kingine ni kile kinachohusu Kamati ya Uteuzi wa Mwenyekiti na Makamu wake ambao kwa mujibu wa muswada itaundwa na Spika wa Bunge la Jamhuri na Spika wa Baraza la Wawakilishi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (AG) na yule wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Waziri wa Katiba na Sheria Tanzania Bara na Waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar na Kiongozi Rasmi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Mkosamali alisema muswada huo wa Mabadiliko ya Katiba unasema mwenyekiti wa muda atakuwa Spika wa Bunge lakini akataka: “Mwenyekiti wa muda atokane na Chama cha Majaji wastaafu maana wao hawafungamani na upande wowote.”
Kuhusu Muswada wa Sheria ya Kura za Maoni, alieleza kuwa unasema wananchi wa Zanzibar watahusika kupiga kura katika mambo 22 ya Muungano yaliyopo katika Katiba ya sasa tu... “Wapigie kura mambo yote yaliyo katika Katiba kwa sababu hii ni ya Jamhuri ya Muungano.”

Pia katika muswada huo, madaftari ya orodha ya wapigakura yatakayotumika ni yaleyale yanayoratibiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Tume ya Taifa ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ambayo bado hayajaboreshwa.
“Kwa Zanzibar ili uandikishwe katika daftari la wapiga kura lazima uwe na vigezo vya ukaazi lakini huku Bara kama Kariakoo kuna Wapemba wengi wafanyabiashara hawa utawatenganisha vipi katika upigaji wa kura?” alihoji.
Alisema miswada hiyo imepangiwa siku mbili na kila mmoja utajadiliwa kwa siku moja, muda ambao alisema ni mdogo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate