Rais Hollande ameyasema hayo mbele ya wanadiplomasia wa kigeni walioko mjini Paris na kudai kuwa, vita na mapambano hayo hayafanyiki dhidi ya dini, bali ni mapambano dhidi ya chuki na uadui. Rais wa Ufaransa amesema kuwa, majeshi ya nchi hiyo yanaendelea kuwasaka watu wanaoshirikiana na makundi ya kigaidi ya al Qaeda na Daesh ambayo yamejitangaza kuwa yana mfungamano na watu waliotekeleza mashambulizi ya Paris. Rais Hollande amesisitiza kwamba, kukaririwa vitisho vya kufanyika operesheni za kulipiza kisasi hakutazuia kutekelezwa operesheni hizo. Rais wa Ufaransa amezitaka nchi za Ulaya kuchukua hatua za pamoja za kukabiliana na makundi ya kigaidi.
Rais Hollande ameyasema hayo mbele ya wanadiplomasia wa kigeni walioko mjini Paris na kudai kuwa, vita na mapambano hayo hayafanyiki dhidi ya dini, bali ni mapambano dhidi ya chuki na uadui. Rais wa Ufaransa amesema kuwa, majeshi ya nchi hiyo yanaendelea kuwasaka watu wanaoshirikiana na makundi ya kigaidi ya al Qaeda na Daesh ambayo yamejitangaza kuwa yana mfungamano na watu waliotekeleza mashambulizi ya Paris. Rais Hollande amesisitiza kwamba, kukaririwa vitisho vya kufanyika operesheni za kulipiza kisasi hakutazuia kutekelezwa operesheni hizo. Rais wa Ufaransa amezitaka nchi za Ulaya kuchukua hatua za pamoja za kukabiliana na makundi ya kigaidi.
No comments:
Post a Comment