Tuesday, June 4, 2013
Nec yapendekezwa kuvunjwa, iundwe tume huru.
Dar es Salaam.
Rasimu ya Katiba Mpya iliyozinduliwa jana na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, imependekeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), ivunjwe na kuunda Tume Huru ya Uchaguzi.
Jaji Warioba alisema Tume Huru ya Uchaguzi itakuwa na wajumbe ambao watateuliwa na Rais na kuthibitishwa na Bunge, baada ya kutuma maombi na kufanyiwa usaili.
Jaji Warioba alisema muundo wa tume hiyo mpya, utahusisha kufutwa kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambayo sehemu ya majukumu yake, yatapelekwa kwenye tume hiyo.
Alitaja sifa za wajumbe hiyo kuwa, mwombaji kutokuwa mwanasiasa, mwanaharakati au kutotokana na taasisi yoyote ya kiraia.
“Majina ya waombaji yatachambuliwa na kamati ya uteuzi ambayo mwenyekiti wake atakuwa ni Jaji mkuu na viongozi wengine sita, ambao ni majaji wakuu wa nchi washirika,
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, maspika wa Bunge wa nchi washirika na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu,” alisema Jaji Warioba.
Jaji Warioba alisema baada ya kamati hiyo kupendekeza majina matatu yanayofaa, yatawasilishwa kwa Rais ambaye atateua mwenyekiti, makamu na wajumbe wengine, kabla majina hayo hayajapelekwa bungeni kwa ajili ya uthibitisho.
Licha ya hilo, Tume Huru ya Uchaguzi itakuwa na mamlaka ya kupokea pingamizi za matokeo ya uchaguzi wa urais ndani ya kipindi ya mwezi mmoja baada ya kutangazwa.
Kwa mujibu wa Katiba ya sasa, Mwenyekiti wa tume hiyo amekuwa akiteuliwa moja kwa moja na Rais bila kuhojiwa au kujadiliwa na Bunge au kamati yoyote.
M2 THE P ANA USHAHIDI WOTE KATIKA KIFO CHA ALBERT MANGWEA.
MBIVU na mbichi sasa zinaweza kujulikana, kinachoombwa ni muda tu, kwani mng’amuzi halisi kuhusu kifo tata cha mwanamuziki mwenye kipaji kikubwa Bongo, Albert Mangwea ‘Ngwea’, yupo kwenye mazingira mazuri kueleza kilichotokea.
KWA NINI ANA USHAHIDI WOTE?
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Mgaza Pembe ‘M2 The P’, ndiye mwenye ushahidi wote kwani aliambatana na Ngwea kila sehemu waliyotembelea mpaka nukta ya mwisho nchini Afrika Kusini.
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Mgaza Pembe ‘M2 The P’, ndiye mwenye ushahidi wote kwani aliambatana na Ngwea kila sehemu waliyotembelea mpaka nukta ya mwisho nchini Afrika Kusini.
M2 The P, alipatwa na matatizo sawa na marehemu Ngwea, isipokuwa
mwenzake ilifikia hatua mbaya na kupoteza maisha huku yeye akibaki
mahututi kwenye chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU)
katika Hospitali ya St. Helen Joseph, jijini Johannesburg nchini humo.
Jambo la faraja ni kwamba, M2 The P yupo vizuri kwa sasa, atakaporuhusiwa kutoka, atajibu maswali mengi tata ambayo yamejitokeza tangu Ngwea alipofariki dunia Juni 28, mwaka huu, nchini humo alipokwenda kwenye shughuli zake.
Jambo la faraja ni kwamba, M2 The P yupo vizuri kwa sasa, atakaporuhusiwa kutoka, atajibu maswali mengi tata ambayo yamejitokeza tangu Ngwea alipofariki dunia Juni 28, mwaka huu, nchini humo alipokwenda kwenye shughuli zake.
JAWABU LA SUMU
Moja ya mambo yanayozungumzwa pembeni ni kwamba
kuna uwezekano mkubwa marehemu Ngwea na M2 The P waliwekewa sumu kwenye
chakula au kupuliziwa ‘laivu’ kisha kutokea yaliyotokea, lengo likiwa
kuwadhulumu mzigo wa fedha nyingi waliokuwa nao, hivyo kupona kwa mmoja
huyo ni matakwa ya Mungu ili awe shahidi namba moja wa kifo cha Ngwea.
“Ni jambo la kumshukuru Mungu jamani, M2 The P anaendelea vizuri sana,
kwa sasa anazungumza. Naamini yeye amepona kwa ajili ya kufichua
kilichofichika nyuma ya kifo cha mwenzake.
“Kama kweli walilishwa
sumu kwenye chakula au walipuliziwa au lolote lile lingine, M2 The P
anajua kila kitu kwani walikuwa wote kwa siku nzima mpaka wanarudi
nyumbani alfajiri kwa safari ya kurudi Bongo.
Mwili wa Ngwair leo mchana
SHIRIKISHO la Muziki Tanzania, limesema kuwa mwili wa aliyekuwa
mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Albert Mangwea ‘Ngwair’, sasa
unatarajiwa kuwasili leo mchana.
Mwili wa msanii huyo aliyefariki Mei 28 nchini Afrika Kusini, umekuwa ukipigwa danadana ujio wake, kila ulipotangazwa.
Rais wa Shirikisho hilo, Ado Novemba, alisema kwamba mwili huo unatarajiwa kuwasili leo majira ya saa nane mchana.
Alisema kwa sasa kila kitu kiko tayari, hivyo mwili ukifika utaagwa
siku utakayofika na baadaye atakwenda kuzikwa nyumbani kwao Kihonda
mkoani Morogoro.
Ngwair, alizaliwa 1982 na nyota yake ilianza kuchomoza katika kundi la East Zoo mkoani Dodoma.
Viti Maalumu vyafutwa, ubunge kuwa na ukomo
Dar es Salaam.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba imependekeza katika rasimu ya Katiba Mpya ukomo wa wabunge na kufutwa kwa nafasi za Viti Maalumu bungeni.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba imependekeza katika rasimu ya Katiba Mpya ukomo wa wabunge na kufutwa kwa nafasi za Viti Maalumu bungeni.
Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Mstaafu Joseph Warioba alisema jana, wanapendekeza kwamba ubunge uwe na ukomo wa vipindi vitatu vya miaka mitano, mitano akimaanisha kwamba kipindi cha mtu kuwa mbunge hakiwezi kuvuka miaka 15.
Rasimu hiyo ya Katiba imependekeza kutokuwapo tena kwa Viti Maalumu na badala yake, imetaka kuwapo kwa nafasi tano za uteuzi zibaki kwa Rais ambazo zitahusisha makundi maalumu ya watu wenye ulemavu pekee.
Jaji Warioba alisema Tume imependekeza kuwapo kwa majimbo 25 ya uchaguzi kwa Tanzania Bara na 20 kwa Zanzibar ambayo kila moja litakuwa na wabunge wawili, mwanamke na mwanamume. Kwa mujibu wa rasimu hiyo, majimbo hayo ni mikoa 25 ya Tanzania Bara na wilaya 10 za Zanzibar. Kwa maana hiyo, Bunge la Muungano litakuwa dogo lenye wabunge 75.
Mwenyekiti huyo alisema, wananchi watakuwa na mamlaka ya kumwondoa madarakani mbunge wao endapo hawataridhishwa na utendaji kazi wake.
Alisema hakutakuwa na uchaguzi mdogo wa wabunge
kwa wabunge watakaopitia kwenye vyama vya siasa na badala yake jimbo
litakapokuwa wazi chama kilichokuwa kikiongoza kitateua atakayeshika
wadhifa huo.
“Uchaguzi mdogo utafanyika pindi tu aliyekuwa akiongoza alitokana na mgombea huru (binafsi) hivyo, Tume huru ya Uchaguzi itatakiwa kuandaa uchaguzi mdogo,” alisema Jaji Warioba.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba jana ilizindua rasimu ya Katiba Mpya -Tanzania mpya.
Dar es Salaam.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba jana ilizindua rasimu ya Katiba Mpya inayopendekeza kuwapo kwa mabadiliko makubwa kwenye mfumo wa utawala, yakiwamo ya kuwa na Serikali Tatu; Shirikisho la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Zanzibar.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba jana ilizindua rasimu ya Katiba Mpya inayopendekeza kuwapo kwa mabadiliko makubwa kwenye mfumo wa utawala, yakiwamo ya kuwa na Serikali Tatu; Shirikisho la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Zanzibar.
Mabadiliko mengine yaliyosheheni kwenye rasimu hiyo ni kufutwa kwa viti maalumu vya ubunge, suala la maadili ya viongozi wa taifa, umri wa urais kubaki kama ulivyokuwa na kuruhusiwa kwa wagombea binafsi katika ngazi zote; urais, ubunge, udiwani mpaka ngazi za mitaa.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba alisema Tume pia imependekeza kuingizwa kwenye Katiba Mpya mambo kadhaa kama Tunu, Dira na Misingi ya Taifa.
“Tulitaka kuifanya rasimu hii iwe fupi kadri iwezekanavyo, lakini kutokana na wingi wa maoni tumeifanya iwe na Ibara 240. Katiba ya sasa ina Ibara 152,” alisema Jaji Warioba na kuongeza:
“Tumeendelea kuitambua misingi mikuu minne ya taifa ambayo ni Uhuru, Haki, Udugu na Amani. Lakini pia tukaongeza misingi mingine mitatu ambayo ni Usawa, Umoja na Mshikamano. Tumependekeza Katiba yetu mpya iwe na misingi saba.”
Jaji Warioba alisema Tume pia imetambua mambo
kadhaa kuwa ni Tunu za Taifa: “Tunu ya kwanza ni Utu. Tunaamini kuwa
watu wote ni sawa, tusiwe na ubaguzi wala tofauti zozote.
Tunu nyingine ni Uzalendo, Uadilifu, Umoja, Uwazi Uwajibikaji na Lugha ya Kiswahili.”
Tunu nyingine ni Uzalendo, Uadilifu, Umoja, Uwazi Uwajibikaji na Lugha ya Kiswahili.”
Jaji Warioba alisema pia kuwa Tume imebainisha
malengo ya Taifa ambayo yatakuwa mwongozo wa Mihimili ya Dola; Serikali,
Bunge na Mahakama.
“Malengo hayo yatakuwa ya aina mbalimbali. Kuna malengo ya kisiasa, kiuchumi, kimazingira na mengine mengi yatakayofafanuliwa baadaye,” alisema.
Jaji Warioba alisema Tume pia imependekeza Katiba ijayo ionyeshe wazi maadili ya kijamii, kiutawala na kiuongozi.
Che Mundugwao kortini kwa wizi wa pasipoti 26

MSANII mahiri wa muziki wa asili nchini, Chigwele Che Mundugwao
(46), na wenzake watatu jana walifikishwa katika mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu Dar es Salaam, wakikabiliwa na mashtaka manne, likiwamo la
wizi wa pasipoti 26.
Che Mundugwao anashtakiwa na wenzake, Ofisa Manunuzi wa Idara ya
Uhamiaji, Shemweta Kilwasha (31), Mhandisi wa Idara ya Zimamoto na
Uokoaji, Kenneth Pius (37), na mfanyabiashara, Ally Jabir (34).
Wakili Mwandamizi wa Serikali, Ladislaus Komanya, mbele ya Hakimu
Mkazi Aloyce Katemana, alidai washtakiwa hao wanakabiliwa na kosa la
kula njama kutenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 384 cha Sheria ya
Kanuni ya adhabu ya mwaka 2002.
Wakili Komanya alieleza kuwa kati ya Aprili 16 na Mei 10, mwaka huu,
Shimweta akiwa ni mtumishi wa umma, makao makuu ya Idara ya Uhamiaji,
aliiba paspoti 26 mali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Komanya alidai kuwa washtakiwa Chigwele, Kenneth na Ally, Mei 30
mwaka huu huko Yombo Makangarawe jijini Dar es Salaam, walikamatwa
wakiwa na pasipoti hizo 26 za wizi.
Kuhusu Che Mundugwao, wakili Komanya alidai kuwa mshtakiwa huyo
Aprili 22, mwaka huu, alikamatwa akimiliki paspoti 12 za watu wengine,
bila ya kuwa na sababu yoyote ya msingi.
Wakili huyo aliendelea kudai kuwa Mei, mwaka huu, Che Mundugwao, pia
alikamatwa na maofisa wa usalama akimiliki pasipoti nyingine mbili
zenye majina ya watu wengine bila ya sababu yoyote ya msingi.
WADUDU NI CHAKULA BORA
Wadudu ni chanzo kikubwa cha protini, mafuta mazuri kiafya, madini na kamba lishe. Aidha, wadudu wameelezwa kuwa ni rafiki wa mazingira na ni rahisi kuwafuga au kuwakamata.
Inakadiriwa na shirika hilo kuwa kiasi cha watu bilioni 2 duniani wanatumia wadudu kama sehemu ya milo yao ya kila siku. Imeshauriwa watu kupendelea kula wadudu kutokana na ukweli kwamba protini inayopatikana kwenye wadudu hao ni bora zaidi kuliko ile inayopatikana kwenye nyama ya kuku, ng’ombe, nguruwe na samaki.
Mbali ya wadudu kuwa ni chanzo kikuu cha protini na mafuta mazuri kama ya samaki (fish oil), lakini pia ni chanzo kizuri cha madini ya kashiamu (calcium), chuma (iron), seleniamu (selenium), zinki (zinc) na Vitamini B.
Kumbikumbi.
WADUDU WA TANZANIA
Kuna aina zaidi ya elfu tisa ya wadudu wanaoliwa sehemu mbalimbali duniani. Lakini kwa nchini
Tanzania, kuna aina kuu mbili za wadudu ambao wanajulikana na kutumiwa kama sehemu ya kitoweo katika familia nyingi nchini, hasa vijijini.
Monday, June 3, 2013
PICHA ZA MWILI WA ALBERT MANGWEHA ULIVYOAGWA LEO NCHINI SOUTH AFRICA
Watanzania waishio nchini South Africa, wamepata nafasi ya kuuaga mwili wa mwanamuziki ALBERT MANGWEA aliefia nchini humo … Hii hapa chini moja ya picha inayoonesha watu wakiaga mwili huo …
Mwili wa Marehemu Ngwair utawasili kesho jijini Dar Es Salaam na kuagwa na fans, marafiki na ndugu katika viwanja vya leaders club, kinondoni kabla ya safari ya kwenda Morogoro, ambapo atazikwa huko karibu kabisa na kaburi la baba yake mzazi …
R.I.P Albert Mangweha.
Muda huu wa saa kumi na Mbili kwa saa za Afrika mashariki
kwa saa za South Africa ni
saa kumi na Moja jioni.....tukiwa bado tupo kwenye majonzi
makubwa yakupotelewa na ndugu yetu
Albert Mangweha.....Baada ya ratiba kupangika watanzania
waishio nchini South Africa
wamepata nafasi ya kuaga mwili wa Albert Mangweha
kuelekea katika safari ya mwisho...wakiongozwa na Msanii
Bushoke na Mtoto wa Mhe. Kingunge Ngombale mwiru
,Kinjeketile wanaosimamia mipango ya kuaga mwili nchini South Africa
ZIFUATAZO NI PICHA 4 WATANZANIA WAISHIO SOUTH
AFRICA WAKIAGA MWILI WA
ALBERT MANGWEHA:
kwa saa za South Africa ni
saa kumi na Moja jioni.....tukiwa bado tupo kwenye majonzi
makubwa yakupotelewa na ndugu yetu
Albert Mangweha.....Baada ya ratiba kupangika watanzania
waishio nchini South Africa
wamepata nafasi ya kuaga mwili wa Albert Mangweha
kuelekea katika safari ya mwisho...wakiongozwa na Msanii
Bushoke na Mtoto wa Mhe. Kingunge Ngombale mwiru
,Kinjeketile wanaosimamia mipango ya kuaga mwili nchini South Africa
ZIFUATAZO NI PICHA 4 WATANZANIA WAISHIO SOUTH
AFRICA WAKIAGA MWILI WA
ALBERT MANGWEHA:
![]() |
| Shugli ya kuaga mwili ikiendelea muda huu nchini South Africa..... |
HATIMAYE CHELSEA IMESIBITISHA JOSE MOURINHO NDIYE KOCHA MPYA.
RASIMU YA KATIBA YAZINDULIWA LEO NA HAYA NI MACHACHE YALIOMO.
ACHE YALIOMO!
-SPIKA NA NAIBU WAKE WASIWE WABUNGE,WALA WASIWE VIONGOZI WA SIASA.
- UWEPO MUUNDO WA SERIKALI TATU.
- MAWAZIRI WASIZIDI KUMI NA TANO (15)
- TUME YA UCHAGUZI IJULIKANE KAMA TUME UHURU YA UCHAGUZI.
-KUSIWE NA UCHAGUZI MDOGO.
- MAWAZIRI WASIZIDI KUMI NA TANO (15)
- TUME YA UCHAGUZI IJULIKANE KAMA TUME UHURU YA UCHAGUZI.
-KUSIWE NA UCHAGUZI MDOGO.
-KIKOMO CHA KUWA MBUNGE KIWE MIAKA MITATU (3)
-KATIBU MKUU KIONGOZI KUSIBITISHWA NA BUNGE.
- MAWAZIRI NA MANAIBU MAWAZIRI WASIBITISHWE NA BUNGE MARA RAIS ANAPOWATEUA.
-MATOKEO YA URAIS YALUHUSIWE KUOJIWA MAHAKAMANI KAMA MTU -ASIPOLIZIKA NDANI YA MWEZI MMOJA MAHAKAMA KUU.
-MGOMBEA APATE ASILIMIA 50%KUTANGAZWA MSHINDI.
KUWEPO NA MGOMBEA BINAFSI
-KATIBU MKUU KIONGOZI KUSIBITISHWA NA BUNGE.
- MAWAZIRI NA MANAIBU MAWAZIRI WASIBITISHWE NA BUNGE MARA RAIS ANAPOWATEUA.
-MATOKEO YA URAIS YALUHUSIWE KUOJIWA MAHAKAMANI KAMA MTU -ASIPOLIZIKA NDANI YA MWEZI MMOJA MAHAKAMA KUU.
-MGOMBEA APATE ASILIMIA 50%KUTANGAZWA MSHINDI.
KUWEPO NA MGOMBEA BINAFSI
Hayo ni baadhi tu ya yale yaliomo sasa hatua inayofata ni Mabaraza ya Katiba kukaa na kuipitia Rasimu hii na kuona kwenye mapungufu kulekebisha kaa tayari kuipata rasimu yote jinsi ilivyo mda mfupi ujao..........!!!!
BREAKING NEWS: AJALI MBAYA YA MAGARI IMETOKEA ENEO LA NANE NANE DARAJANI UYOLE MBEYA , YAJERUHI NA WATU WANNE WAHOFIWA KUFA
TAMKO LA BALOZI WA TANZANIA WA AFRICA YA KUSINI KUHUSU KUCHELEWA KUFIKA KWA MWILI WA MAREHEMU NGWAIR TANZANIA.
Balozi wa Tanzania Africa ya Kusini Radhia Msuya.
Balozi wa Tanzania Africa ya Kusini kwenye picha hapo juu ametoa pole
kwa familia,wasanii na wadau wote kwa kupotelewa na kijana ambaye bado
watu walikuwa wanamuhitaji.Amesema kuwa mwili wa marehemu Ngwair
umechelewa kufika Tanzania kutokana na post mortem na taratibu za kupata
kibali cha kusafirisha mwili huo kutoka Serikali ya Africa ya
Kusini.Radhia alisema kuwa kama taratibu zote zitaenda sawa mwili huo
utawasili siku ya Jumanne Tanzania.MSIKILIZE hapo chini;Habari na Anna Peter Blog.
SALAMU ZA RAMBIRAMBI TOKA KWA WIZARA YA HABARI,VIJANA,UTAMADUNI NA MICHEZO KUTOKANA NA KIFO CHA MANGWEHA
Subscribe to:
Posts (Atom)
HABARI MBALIMBALI
‘Dk. Cheni’
‘Sharo Milionea
‘Thea’
African Women
AGNESS MASOGANGE
AK CLASSIC COSMETICS
ALI KIBA
Amanda Poshy
Ant
ANT LULU
Ashley Toto
Aunt Ezekiel
Aunty Ezekiel
AUNTY LULU
Azam Fc
Baby Madaha
BAHATI BUKUKU
Barnaba
BATULI
BBA
Beauty of the day
Belle 9
BI KIDUDE
BIBI BOMBA
Big Brother
Big Brother Africa
Bill Gates
BINTI KIZIWI
BOB JUNIOR
Bodi ya Filamu
Bongo Movie
Bongo Movies
CCM
CHADEMA
Chombezo
Christina Shusho
Chuchu hans.
Clouds Media Group
Club Bilicanas
DAR LIVE
DAVINA
Dayna Nyange
Diamond
Dida
Diva Loveness Love
Dj Ommy Crazy wa Maisha Club
DOGO JANJA
DOKI
DR.CHENI
DSTV
Dude
Dully Sykes
EBSS 2013
Elizabeth Michael
Epiq Bongo Star Search (EBSS)
ESHA BUHETI
Ester Bulaya
Feza Kessy
FIESTA 2014
Flaviana Matata
FLORA MBASHA
FLORA MVUNGI
Francis Cheka
GARDNER
GLOAL PUBLISHERS
GLOBAL TV ONLINE
H. BABA
Halima Mdee
HAMISA
Happy birthday
Hemedi
Hemedy Suleiman
HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE
Hoyce Temu
Huddah Monroe
HUSINA
IRENE PAUL
Irene Uyoya
ISABELLA
J film 4 life
Jack Chuz
JACK PATRICK
Jacob Steven ‘JB’
Jacqueline Dustan
JACQUELINE WOLPER
Jaji Khamis 'Kashi'
Jay Dee
JENNIFER KYAKA (ODAMA)
JIDE
JINI KABULA
JK
JO
Johari
Jokate Mwigelo ‘Kidot’.
JOTI
Joyce Kiria
Joyce Kiwia
JUX
K-LYNN
KADINDA
kaja
Kajala Masanja
Kapotive Star Singers
KATUNI
Kemmy
Kero Zetu
KHADIJA OMAR KOPA
KIKWETUKWETU
KILI MUSIC AWARDS
KOLETA
Lady Jay Dee
Lady Jaydee
Lake Oil
LAVEDA
Linah Sanga
Linex
Lisa Jensen
Loveness Diva
Lucy Francis Komba
Lulu
M2 The P
MABILIONEA
Madam Rita
MADELA
Magazeti
Mahusiano
Maimartha Jesse
MAINDA
MAISHA
Makala
Malkia Elizabeth
MAMTEI
MANDELA
MARIAM ISMAIL
Masanja Mkandamizaji
Mashindano ya Miss Tanzania
Matangazo
Matonya
MaxMalipo
MAYA
MELLIS EDWARD
MENINAH
MGOSI MKOLONI
Mh Halima Mdee
mic
Michezo
MILLEN HAPPINESS MAGESE
MISS CHANG'OMBE
MISS DAR CITY CENTER
Miss East Africa
MISS REDD'S IRINGA 2013
MISS TANGA 2013.
MISS TANZANIA 2014
Miss Tanzania mwaka 2011
MISS TEMEKE 2014
MISS USTAWI
MISS UTALII TANZANIA 2012/13
Miss vyuo vikuu 2013
MKALA
MREMBO HUDDAH
Mrisho Mpoto
Mrisho Ngassa
MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES.
MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013
Mtitu
muziki
Mwana FA
MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Mzee Majuto
Nancy Sumari
Nani Mtani Jembe?
NAPE
Nassoro ‘Nora’
Natasha
Nay wa Mitego
Necta
Nelly Kamwelu
NEY WA MITEGO
Nisha
NSSF;Zantel
Nyamwela
NYimbo
Nyota yako
OBAMA TANZANIA
OMMY DIMPOZ
P FUNK
PAM D
Peniel Mgilwa ‘Penny’
PETIT MAN
Profesa Jay
Q - CHILA
Q Boy
Q Chilla
QUEEN DARLEEN
RACHEL NDAUKA
RAIS KIKWETE
Rais Kikwete.
Rasimu Ya Katiba TZ
Ray
Ray C
Redd’s Miss IFM
REDD'S MISS KAGERA 2013
REDD'S MISS TZ
REDDS MISS TANZANIA 2014
Redds Miss wa Mikoa
REHEMA FABIAN
RICHIE RICHIE
Rihanna
ROSE MUHANDO
Rose Ndauka
Ruge Mutahaba.
SABASABA 2013
Saida Karoli
Saikolojia
Sajeti
SAJUKI
Sandra
SHAA
Shamsa Ford
Sheikh Ponda
Shilole
Sintah
Siwema
Skin Tricks
Snura Mushi
Spika Makinda
staa
Staa Wetu
Stella Mwangi
STYLE ZA NYWELE
Taifa Stars
Tamasha la matumaini
TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013
Tangazo
TANZANIA
TEGO
TENGENEZA WEBSITE NA BLOG
TID
Tundaman
Tupo wangapi?
TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Twanga Pepeta
USA PAGEANT 2014
VAI
Wastara
WEMA
WEMA SEPETU
Yanga
Yanga Bingwa 2013
YOUNG D
Yvonne Cherry ‘Monalisa’
Z Anton.
Zari
Zito kabwe









