EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, August 14, 2012

Dk Ulimboka awekwa mafichoni

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Stephen Ulimboka baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere Dar es Salaam juzi akitokea Afrika Kusini alikokuwa akitibiwa.Picha na Fidelis Felix
YABAINIKA HAYUPO NYUMBANI, TAARIFA ZAKE ZAFANYWA SIRI, BABA, NDUGU, MARAFIKI WAGOMA KUZUNGUMZA
Waandishi Wetu
WINGU limegubika sakata la kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari Nchini, Dk Steven Ulimboka siku moja baada ya kurejea nchini, huku watu wake wa karibu akiwamo baba mzazi, wakigoma kusema chochote kumhusu.
Dk Ulimboka alirejea nchini juzi akitokea Afrika Kusini alikokuwa amelazwa kwa ajili ya matibabu kwa takriban mwezi mmoja na nusu, baada ya kutekwa, kuteswa na kutupwa kwenye Msitu wa Pande nje kidogo na Jiji la Dar es Salaam usiku wa kuamkia Juni 26 mwaka huu.
Ingawa wakati wa ugonjwa wake baadhi ya watu wake wa karibu walikuwa wakitoa maelezo mbalimbali, jana wote waligoma kusema chochote, huku jitihada za gazeti hili kumpata nyumbani kwake zikigonga mwamba.
Baba mzazi wa Dk Ulimboka, Stephen Mwaitenda aliweka wazi kuwa ni vigumu kumwona daktari huyo jana.
Takriban watu wote waliofika nyumbani kwa Mzee Mwaitenda jana kumjulia hali Dk Ulimboka waliambiwa kuwa hayupo nyumbani.
Mwaitenda alilieleza gazeti hili kuwa ana furaha kuwa mtoto wake alirejea nchini salama licha ya kupelekwa Afrika Kusini akiwa taabani kutokana na kipigo.
Alipotakiwa kueleza juu ya kile kilichompata, mtoto wake huyo alisema: "Mungu na Steven mwenyewe (Dk Ulimboka) ndio wanaojua kilichotokea."
Aliongeza: “Kweli nimefurahi kwamba mwanangu amerudi, lakini siwezi kuelezea nini kilimtokea alipotekwa," alisema Mwaitenda.
Alisema Dk Ulimboka hayupo nyumbani na hajui kwamba angerudi wakati gani. "Hata kama angekuwapo, ni vigumu kumwona," alisema.
Kauli ya Katibu wa Madaktari
Katibu wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Edwin Chitage alisema madaktari walikuwa hawajaamua nini kingefuata baada ya Dk Ulimboka kurejea nchini.
Alisema hata hivyo, daktari huyo anahitaji muda wa kupumzika kwanza na familia yake.
“Aliporudi jana (juzi) alitumia muda wake kukaa na familia yake, mpaka sasa hatujajua hatua inayofuata. Dk Ulimboka atazungumza wakati mwafaka ukifika,” alisema Dk Chitage.
Rais wa Chama cha Madaktari (MAT), Dk Namala Mkopi hakutaka kuzungumzia suala hilo akieleza kuwa alikuwa mkutanoni.
Dk Mkopi alitoa kauli hiyo baada ya daktari aliyemtibu Dk Ulimboka wakati wa tukio la kutekwa, Profesa Joseph Kahamba akiwa amesema yeye (Mkopi) ndiye angesaidia  kupatikana kwa Dk Ulimboka ili azungumze na waandishi wa habari.
Dk Chitage alipoulizwa nini kinaendelea baada ya Dk Ulimboka kurejea nchini alijibu, "Hakuna kinachoendelea."

Aliendelea, "Leo hakuna kitu, tumepumzika na hata yeye tumemwacha apumzike na familia yake," alisema Dk Chitage.

Alisema Jumuiya hiyo na familia yake wanaandaa mazingira yatakayowezesha Dk Ulimboka kuzungumza na umma kupitia vyombo vya habari.

"Kuhusu hatua zitakazofuata tutaandaa utaratibu na tutawaarifu, juu ya hatua zipi tutachukua ikiwamo hili linaloumiza vichwa vya wengi la mazingira ya kutekwa kwake," alisema Dk Chitage.

Katibu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Rodrick Kabangila alipoulizwa kuhusu suala hilo alisema yuko safarini na hajui kinachoendelea.

"Nipo Mwanza, nimesafiri na sijui kinachoendelea," alisema.

Alisema MAT itakutana kujadili suala hilo wakati wowote na kwamba utaratibu utaandaliwa kwa Dk Ulimboka kuzungumza na vyombo vya habari.

"Unajua sisi tuliomba kibali cha kuandamana kushinikiza Serikali kuunda tume huru kuchunguza tukio hilo na kuwabaini waliohusika tukakataliwa. Lakini sasa yeye amerudi na anawajua waliomdhuru. Tutaandaa utaratibu,  atazungumza nanyi ili watu wote wajue," alisema Dk Kabangila.

Mkurugenzi wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake (Tamwa), Ananilea Nkya, alisema hakuwa na mawasiliano yoyote na Dk Ulimboka wala hajui kinachoendelea baada ya kuachana naye juzi Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere.

Polisi wazungumza

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova akizungumza kupitia msaidizi wake, alisema kuwa suala la Dk Ulimboka limefungwa na hawezi kulizungumzia tena kwa kuwa lipo mahakamani.

"Kamanda alikwishasema kuwa suala hilo lipo mahakamani hivyo hawezi kulizungumzia," alisema msaidizi huyo.

Alipoulizwa iwapo polisi ilikubali maombi ya madaktari kutaka tume hiyo ivunjwe na iundwe nyingine huru alijibu, "Tume  inaendelea na kazi."

"Tume inafanya kazi yake na polisi pia wapo katika kazi zao," alisema na kukata simu.

Wanasiasa
watoa wito

NCCR-Mageuzi, CUF na Democratic (DP) vimemtaka Dk Ulimboka kuwataja watu waliomteka na kumpiga.

Wito huo ulitolewa jana kwa nyakati tofauti na Katibu Mkuu wa NCCR-, Samwel Ruhuza, Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro  na Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila.

“Atumie roho yake na dhamira yake kuwataja watu waliomfanyia unyama ule ili jamii ijue na pengine ndio utakuwa mwisho wa watu kufanyiwa vitu vya aina hii,” alisema Ruhuza.

Ruhuza alisema kuwa kiongozi huyo wa madaktari amerejea huku akiwa na afya njema, lakini bado ana deni kwa watu wasiopenda vitendo vya unyanyasaji.

“Ndiyo maana nikasema azungumze jambo hili kutoka ndani ya moyo wake,” alisema Ruhuza.

Mtikila alisema licha ya kwamba Dk Ulimboka anatakiwa kuwataja waliomfanyia vitendo hivyo, yaliyomkuta yanatakiwa kupelekwa katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki za Binadamu.

“Nimeshazungumza na mtu mmoja kutoka mjini London, Uingereza amesema kuwa jambo hilo linawezekana,”  alisema Mtikila.

Alifafanua kwamba, atafanya kila njia ili akutane na Dk Ulimboka na kumshawishi akafungue kesi katika mahakama hiyo ili liwe fundisho kwa wanaopenda kuwanyanyasa Watanzania wanaodai haki zao.

“Nitafanya kila njia ili nionane na Ulimboka, hili jambo ni lazima lifike katika mahakama ya kimataifa ya haki za binadamu…, pia anatakiwa kuwataja waliomfanyia unyama huu,” alisema Mtikila.

Kwa upande wake, Mtatiro alisema kuwa Ulimboka anatakiwa kukutana na vyombo vya habari na kueleza mambo yote ili kufichua yaliyokuwa yakifichwa na vyombo vya usalama.

“Ukweli utamweka huru na utawaweka huru watu wengi ambao wanaweza kufanyiwa unyama siku zijazo. Ikiwezekana afungue kesi ili haki itendeke,” alisema Mtatiro na kuongeza:

“Ulimboka anatakiwa kufahamu kwamba Watanzania hawakukubaliana na mateso aliyopewa, unyama aliofanyiwa unalaaniwa na kila mtu,” alisema Mtatiro.

Habari hii imeandikwa na Fidelis Butahe, Aidan Mhando, Joseph Zablon,  Geofrey Nyang’oro, Boniface Meena na Leon Bahati

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate