EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, August 18, 2012

Serikali yawaangukia Waislamu

WAKATI shinikizo la baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu kutaka kususia sensa likishika kasi, serikali imewaomba radhi Waislamu kutokana na matangazo yaliyorushwa na Kituo cha Televisheni ya Taifa (TBC), yaliyoonesha kwamba idadi ya Wakristo nchini ni kubwa kuliko Waislamu.
TBC ilirusha matangazo hayo siku ya Sikukuu ya Muungano (Aprili 26) mwaka huu na kuonesha idadi ya Wakristo ni asilimia 52, Waislamu asilimia 32 na madhehebu mengine asilimia 14.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa TBC, Clement Mshana alisema kuwa matangazo hayo yalitolewa kwenye mtandao wa 
Wikipedia na kurushwa hewani kimakosa.
Alisema baada ya kurushwa kwa matangazo hayo kimakosa, TBC walipokea barua nyingi kutoka Chama cha Wanataaluma wa Kiislamu Tanzania (Tanzania Muslim Professional Association) zikieleza kukerwa na taarifa hiyo.

Mshana Alisema katika barua hiyo, chama hicho kilitaka ufafanuzi jinsi takwimu hizo zilivyopatikana na TBC iwaombe radhi Watanzania.
Alisema Mei 15, TBC ilimwandikia barua Katibu Mkuu wa chama hicho cha Waislamu, Pazi Mwinyimvua na kuomba radhi kwa kasoro iliyotokea na kueleza kwamba shirika lake limemwonya mfanyakazi aliyerusha hewani takwimu hizo kimakosa.

“Nichukue fursa hii tena kuwaomba radhi ndugu zetu wa dini ya Kiislamu kutokana na maumivu waliyopata kutokana na takwimu hizo. Na kwa kuwa huu ni mwezi mtukufu wa Ramadhani na moja ya mahitaji wakati wa mfungo ni kusameheana, naomba waumini wote wa dini ya Kiislamu wapokee kwa moyo wa upendo ombi hili la kuwataka radhi,” alisema Mshana.

Aliongeza kwamba kwa kuwa suala hili limehusishwa na sensa ya watu na makazi, anawaomba waumini wa dini ya Kiislamu kusamehe kilichotokea na washiriki katika sensa ya watu na makazi itakayofanyika Agosti 26, mwaka huu.
Wakati serikali ikiendelea kuhimiza wananchi kushiriki sensa, kuna kundi la Waislamu limejitokeza kupinga tukio hilo.
 Walimu 108 waenguliwa kwenye semina ya Sensa Dar
 Kundi hilo limekuwa likipita sehemu mbalimbali nchini kueneza sumu ya kuwataka Waislamu wasishiriki sensa kwa madai kuwa serikali imelenga kuwabagua kwa kutangaza takwimu zinazoonesha Wakristo ni wengi zaidi ya Waislamu.
Mmoja wa viongozi wa kundi hilo, Issa Sadick, hivi karibuni alizitaja baadhi ya sababu za kukataa kuhesabiwa kuwa ni serikali kuendelea kuwabagua Waislamu katika miradi mbalimbali ya maendeleo.

Hata hivyo Sheikh Mkuu Mufti Shabaan bin Simba hivi karibuni aliwataka Waislamu kushiriki sensa na walipuuze kundi la masheikh linalozunguka nchini kutaka wasusie.
Wakati huo huo, walimu 108 walioteuliwa kuhudhuria semina ya makarani wa sensa, wameenguliwa na nafasi zao kuzibwa na watu wengine.
Utafiti wa gazeti hili umebaini kuwa, walioenguliwa ni walimu wa Kituo cha Mafunzo cha Sekondari Tambaza jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa habari hizo, walimu hao wameenguliwa kutokana na kushindwa kufanya vizuri kwenye mtihani wa majaribio.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, baadhi ya walimu hao walisema wanapinga kuondolewa kwao kwani walikwishakubaliana katika mkataba wa malipo, na tayari walishaanza mafunzo kwa ajili ya kazi ya ukarani wa sensa.

Walisema kuwa wahusika wamekuwa wakiwaleta ndugu zao na kuwapunguza walimu ambao tayari walishaanza mafunzo kwa siku nne sasa.
Walimu hao walisema wanaitaka serikali iwalipe fedha zao za siku nne ambazo tangu waanze mafunzo hayo hawajalipwa.
Taarifa hii imeandaliwa na Zawadi Chogogwe, Agness Newa na Stella Mushi wa Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate