EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, December 21, 2012

Makundi kwenye kombe la Afrika 2013

 Afrika kusini inawania taji lake la pili

     Afrika kusini inawania taji lake la pili

Baada ya Libya kutumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe, shirikisho la soka barani Afrika liliamua mwaka jana kuwa fainali za mwaka 2013 zifanyike nchini Afrika kusini. Timu ya nchi hiyo kama inavyojulikana "Bafana Bafana", inaweza kutwaa taji hilo kwa mara ya pili baada ya kuwa mabingwa mwaka 1996. Afrika kusini imo katika kundi A pamoja na Angola, Cape Verde na Morocco.
Angola yatumai kufanya vizuri mara hii
Kwa mara ya saba Angola imefanikiwa kucheza katika fainali za kombe la Afrika. Timu hiyo inayofahamika kama "Palancas Negras", ilifanikiwa kwa kuiondoa Zimbabwe kwa mabao 3-1 katika mchezo wa kwanza na kuiadhibu Zimbabwe tena kwa mabao 2-0 nyumbani mjini Luanda. Magoli yote mawili yalifungwa na mshambuliaji Manucho (kulia).
 Angola yatumai kufanya vizuri mara hii

Mashabiki wa Angola wameonyesha matumaini kuwa timu yao (pichani) itafanikiwa kuvuka kikwazo cha duru ya kwanza. Wanahisi kuwa ushindi unawezekana dhidi ya wenyeji Afrika kusini, Morocco na Cape Verde. Kocha wa Angola, raia wa Uruguay, Gustavo Ferrín, kwa upande wake analiona kundi A kuwa gumu zaidi.                      Côte d'Ivoire haitakubali tena kuwa ya pili

Côte d'Ivoire inakwenda katika fainali hizo nchini Afrika kusini ikiwa ni makamu bingwa. Côte d'Ivore imeishinda Senegal katika awamu ya kufuzu katika makundi. Mjini Dakar baada ya Côte d'Ivoire kuongoza kwa mabao 2-0, kulizuka ghasia na mchezo kuvunjika. Senegal iliondolewa. Côte d'Ivoire inacheza katika kundi D pamoja na Tunisia, Algeria na Togo.
Côte d'Ivoire haitakubali tena kuwa ya pili 
                                                       Togo: Timu yenye wasiwasi
Mara sita Togo imeshiriki katika fainali za kombe la Afrika, na mwaka 2006 ilishiriki katika fainali za kombe la dunia nchini Ujerumani. Mwaka 2010 timu hiyo ilijitoa katika fainali zilizofanyika nchini Angola baada ya basi la timu hiyo kushambuliwa na waasi wanaotaka kujitenga katika jimbo la Cabinda. Watu watatu walikufa. Togo imo katika kundi D pamoja na Côte d'Ivoire, Tunisia na Algeria.
 Togo: Timu yenye wasiwasiNiger yashiriki kwa mara ya pili
Baada ya kushiriki kwa mara ya kwanza mwaka 2012 Niger inarejea nchini Afrika kusini kwa mara ya pili.Timu hiyo inayojulikana kama "Menas", kwa lugha ya Kihausa, ina maana ya mnyama paa. Mlinzi Mohamed Chocoto (pichani) anayechezea timu ya AS Marsa ya Tunisia ni mmoja kati ya wachezaji maarufu wa timu hiyo. Niger imo katika kundi B ikiwa pamoja na Ghana, Mali, na Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo.
         Morocco: Simba wa milima ya Atlas
"Simba" iliisambaratisha Msumbiji kwa mabao 4-0 mjini Marrakesh na kufanikiwa kukata tiketi yao kwa fainali hizo za Afrika kusini. Morocco katika mwaka 1986 ilikuwa timu ya kwanza ya kiafrika kuwa mshindi wa kundi lake katika kombe la dunia, dhidi ya Uingereza, Poland na Ureno. Mwaka 1976 ililitwaa kombe la Afrika. Morocco imepangwa katika kundi A pamoja na Afrika kusini, Angola na Cape Verde.
Tunisia: Mshiriki wa kila mara
Kwa mara ya 15 Tunisia imekuwa katika fainali za kombe la Afrika. Mwaka 2004 Tunisia ilishinda taji hilo ikiwa mwenyeji wa mashindano hayo. Mwaka 1978 Tunisia iliandika historia kwa kuishinda Mexiko kwa mabao 3-1 katika fainali za kombe la dunia huko Argentina. Ilikuwa ushindi wa kwanza katika kombe la dunia kwa timu ya kiafrika. Tunisia imo katika kundi D pamoja na Côte d'Ivoire, Algeria na Togo.
 Burkina Faso inataka kuonyesha maajabu
Burkina Faso si vigogo wa soka barani Afrika. Matokeo mazuri kwa timu hiyo yamepatikana katika fainali za 1998 iliposhika nafasi ya nne. Tangu 1996 Burkina Faso imefanikiwa kila mara kufuzu kucheza katika fainali. Nyota wa timu hiyo ni mshambuliaji Moumouni Dagano (pichani) anayecheza nchini Qatar katika timu ya Al-Sailiya. Burkina Faso imo katika kundi C pamoja na Zambia, Nigeria na Ethiopia.

                       Wageni wa mashindano hayo Cape Verde

Wacape Verde wanajisikia fahari na kikosi chao cha "Nyangumi wa Buluu", ama kama wanavyofahamika nchini humo "Tubarões Azuis". Kwa mara ya kwanza nchi hiyo inashiriki katika mashindano makubwa ya kimataifa. Januari 19 Cape Verde itafungua dimba la fainali hizo dhidi ya wenyeji Afrika kusini mjini Johannesburg.
 Wageni wa mashindano hayo Cape Verde
                                                                  Cape Verde
Cape Verde iliitoa mashindanoni vigogo wa soka barani Afrika, Simba kutoka Cameroon kwa kuwapiga mabao 2-0 mjini Praia kutokana na uwezo wa kocha Lúcio Antunes. Ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa marudio haukunusuru Simba. Cape Verde hata hivyo inakabiliwa na kazi ngumu dhidi ya Afrika kusini, Morocco na Angola katika kundi A. Kuna uwezekano mkubwa wa kuaga mashindano katika duru ya mwanzo.

                         Ghana yawania taji lake la tano

Mara nne Ghana imekuwa mabingwa wa Afrika. Mara nane timu hiyo ya Afrika magharibi imejikuta katika fainali. Mara ya mwisho ilikuwa nchini Angola mwaka 2010. Ghana ilishindwa na Misri kwa bao 1-0. Mchezaji maarufu katika timu hiyo alikuwa mchezaji wa kati André Ayew (kulia) kutoka Olympique Marseille. Ghana imo katika kundi B pamoja na Mali, Niger na Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo.
 Ghana yawania taji lake la tano
                                                                           Timu ya Ghana

              Nigeria: Kiwango cha juu tangu miaka kadhaa

"Tai wa kijani", ni moja kati ya timu bora kabisa barani Afrika. Mwaka 1994 Nigeria ilifikia nafasi ya tano katika orodha ya FIFA ya timu bora duniani, ikiwa ni kiwango bora kabisa kwa timu kutoka Afrika hadi sasa. Mwaka 1980 na 1994 Nigeria ilishinda kombe hilo la Afrika. Ilishika nafasi ya tatu mwaka 2002, 2004, 2006 na 2010. Nigeria imo katika kundi C pamoja na Zambia, Burkina Faso na Ethiopia.
 Nigeria: Kiwango cha juu tangu miaka kadhaa
                                                                     Mali inakuja juu
Mali imetumbukia katika matatizo ya kisiasa kutokana na kujitenga kwa upande wa kaskazini unaodhibitiwa na makundi ya Waislamu wenye imani kali. Pamoja na hayo, Mali imefanikiwa kukata tiketi ya fainali za 2013. Katika fainali za 2012 nchini Guinea ya Ikweta na Gabon, timu hiyo ilifanikiwa kushika nafasi ya tatu. Mali imo katika kundi B pamoja na Niger, Ghana na Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo.
 Mali inakuja juu
                                                   Burkina Faso inataka kuonyesha maajabu
Burkina Faso si vigogo wa soka barani Afrika. Matokeo mazuri kwa timu hiyo yamepatikana katika fainali za 1998 iliposhika nafasi ya nne. Tangu 1996 Burkina Faso imefanikiwa kila mara kufuzu kucheza katika fainali. Nyota wa timu hiyo ni mshambuliaji Moumouni Dagano (pichani) anayecheza nchini Qatar katika timu ya Al-Sailiya. Burkina Faso imo katika kundi C pamoja na Zambia, Nigeria na Ethiopia. Burkina Faso inataka kuonyesha maajabu
                                                                Burkina Faso
                                        Ethiopia inakabiliwa na changamoto kubwa
Kwa muda wa chini ya mwaka mmoja kocha Sewnet Bishaw amefanikiwa kuiwezesha Ethiopia kufuzu kucheza katika fainali za kombe la Afrika ambapo kwa muda wa miaka 31 Ethiopia ilishindwa kushiriki. Mwaka 1962 Ethiopia ilitawazwa mabingwa wa Afrika, wakati mashindano hayo yalipofanyika nchini humo. Pamoja na mabingwa watetezi Zambia, Nigeria na Burkina Faso, Ethiopia inarejea dimbani katika kundi C.
 Ethiopia inakabiliwa na changamoto kubwa

                      Kongo: Urithi wa uchawi wa soka

Mwaka 1974 wakati huo ikiitwa Zaire nchi hiyo iliandika historia, ikifanikiwa kama timu ya kwanza kutoka Afrika kusini mwa jangwa la Sahara kufuzu kucheza katika fainali za kombe la dunia. Wakati huo ilishakuwa bingwa wa kombe la Afrika mara mbili, mwaka 1968 na 1974. Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo inaingia katika fainali za mwaka 2013 kikiwa katika kundi B pamoja na Ghana, Mali na Niger.
 Kongo: Urithi wa uchawi wa soka

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate