EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, December 21, 2012

Maoni ya wahariri juu ya Zuma na Ngudjolo Chui.

Wahariri wanatoa maoni juu ya kuchaguliwa tena kwa Jacob Zuma kuwa Rais wa chama cha ANC na pia juu ya aliyekuwa mbabe wa kivita katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Ngudjolo Chui
 Zuma achaguliwa tena kuwa Rais wa ANC
Kuhusu kuchaguliwa tena kwa Jacob Zuma na hivyo kuendelea kuwa Rais wa chama tawala nchini Afrika Kusini, ANC, gazeti la "Süddeutsche" linasema licha ya mwanasiasa huyo kuchaguliwa kwa kishindo, Afrika Kusini imo katika mgogoro mkubwa. Mhariri wa gazeti hilo anasema sababu ya mgogoro huo ni kashfa na udhaifu uliomo katika uongozi wa Zuma. Gazeti linasema Afrika kusini ilikabiliwa na migomo iliyoandamana na umwagikaji wa damu. Hali hiyo ilisababisha hasara katika uzalishaji na kuiathiri sekta ya uchumi.

Gazeti la "Stuttgarter" linasema, chama cha ANC kinaweza kugawanyika katika siku za usoni kutokana na kushindwa kuzitimiza ahadi nyingi kilizozitoa kwa wafuasi wake.Mhariri wa gazeti hilo anafafanua kwa kusema mpaka sasa chama cha ANC bado kinaungwa mkono na mamilioni ya watu. Sababu ni kwamba kwa mamlioni ya waaafrika chama cha ANC kimeleta ukombozi. Lakini ahadi ambazo chama hicho kilizitoa kwa mamilioni ya wananchi bado hazijatekelezwa mpaka leo.

Watu wengi hawana ajira, na idadi yao inaongezeka,mfumo wa elimu kwa ajili ya waafrika una mapungufu. Mamilioni ya waafrika wanaendelea kuishi katika vitongoji vya masikini. Kwa hivyo kuchaguliwa tena kwa Zuma kukiongoza chama cha ANC, kunaweza kusababisha mpasuko ndani ya chama hicho.
"Mbabe wa kivita Ngudjolo Chui aachiwa"

Mahakama ya kimataifa ya mjini The Hague ICC jana ilimwachia huru ,aliekuwa mbabe wa kivita Ngudjolo Chui aliefikishwa mbele ya mahakama hiyo kujibu mashtaka ya kutenda uhalifu dhidi ya ubinadamu na uhalifu wa kivita katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. Lakini hakupatikana na hatia.
Juu ya hukumu hiyo gazeti la "Neue Osnabrücker" linasema:"Jambo moja ni la uhakika: uhalifu ulifanyika katika kijiji cha Bogoro mashariki mwa Kongo. Watu waliuawa,wengine walichomwa moto wakati wakiwa hai, na wanawake walibakwa. Lakini Ngudjolo Chui hakupatikana na hatia ya mashtaka hayo" Gazeti la "Neue Osnabrücker " linasema hukumu hiyo inathibitisha kwamba Mahakama ya mjini The Hague, ICC inafanya kazi yake . Hatahivyo waendesha mashtaka wanayo haki ya kukata rufaa.
Mhariri wa "die tageszeitung" anakubaliana na mtazamo huo na anasema: Mahakimu wa ICC wamebainisha kwamba mashtaka yaliyomkabili Chui yalikuwa na mashaka-mashahidi wengi hawakuwa wazi katika kauli zao-walibabaika na hawakuaminika. Katika hali hiyo mshtakiwa hawezi kutiwa hatiani.Ni sahihi kabisa kwamba mahakimu wametoa haki pia kwa mbabe wa kivita.
CHANZO CHA HABARI NA IDHAA YA KISWAHILI DW.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate