EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, December 11, 2012

UTAJIRI WA MZEE WA UPAKO NI TISHIO.


Na Mwandishi Wetu
MCHUNGAJI wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo, maarufu kwa jina la Mzee wa Upako ametamba kwamba yeye ni tajiri tishio kuliko watumishi wenzake kwani anamiliki magari sita ya kifahari na nyumba ambayo ina kiyoyozi (AC).
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo 'Mzee wa Upako'.
Akihubiria waumini wake kanisani hapo juzikati, Ubungo- Kibangu, jijini Dar es Salaam na kuoneshwa na Kituo cha Runinga cha C2C na Channel Ten hivi karibuni, Mzee wa Upako alisema magari yake hayo ya kifahari yote yana viyoyozi na si ya kutoka Japan, akimaanisha ya gharama kubwa zaidi.
“Mimi ndiye Mzee wa Upako, nikitoka nje nakuta magari yote sita yapo, nachagua leo niendeshe hili au lile. Najiambia hapana hili nililiendesha jana, nachukua lingine,” alitamba kiongozi huyo.
Mercedes Benz.
Aliyataja magari hayo kuwa ni Mercedes Benz, Land Rover Discovery, Range Rover Sport, BMW X5, Ford Escape na Range Rover Vogue ambayo Uwazi linatafiti bei zake na kuwapelekea wasomaji siku zijazo.
Aidha, mtumishi huyo wa Mungu aliendelea kutamba kuwa nyumbani mwake mna viyoyozi ‘vikali vya kufa mtu’ na kubainisha kwamba huwa akitoka kwenye gari lenye kiyoyozi anaingia katika nyumba yenye kiyoyozi.
“Mimi nasema hayo kwa sababu ni mlipaji mzuri wa kodi za serikali, sioni sababu ya kuficha mali zangu, kwa nini nifiche?” alihoji na kuongeza:
 
Land Rover Discovery.
“Magari yote nimeandika kwa jina langu ili niyalipie kodi, situmii mwamvuli wa kanisa kwa kukwepa kodi.”
Aliwaambia waumini wake kuwa kazi yake ni kugawa upako wa baraka za utajiri na kwamba kupitia kanisa lake watu wengi wameneemeka kimaisha.
“Nasisitiza kuwa kila mtu anatakiwa kuwa tajiri lakini utajiri wa halali siyo ule wa kudhulumu, ndiyo maana nasimama hapa kutaja mali zangu, magari hayo si mali ya kanisa ni yangu,” alisema.

 
BMW X5.
Pia aliyachambua makanisa kwa kusema: “Makanisa yetu haya ya kiroho ni hovyo, wameingia matapeli na ninayasema haya kwa kuwa ninayajua, nipo ndani, ndiyo maana najua kitu ninachokisema na mtu akitaka tubishane kwa hoja hii hawezi kunishinda.
“Najua hili ninalozungumza ni jambo zito na sasa ninaposema haya maneno ni sauti ya Mungu mwenyewe inatoka kupitia kinywa changu.”
Mzee wa Upako aliwahi kusema kwamba amekuwa akitumia zaidi ya shilingi 300,000,000 kwa mwaka kwa ajili ya kuendesha vipindi vyake katika runinga na fedha hizo huchangisha kupitia akaunti zake, akasisitiza vipindi vya runingani ni mali yake na si kanisa.
 
Ford Escape.
Wachambuzi wa mambo wameichambua hesabu hiyo na kugundua kwamba mchunga kondoo huyo hutumia zaidi ya shilingi 25,000,000 kwa mwezi kulipia vipindi hivyo.
Kiongozi huyo ana kanisa kubwa la ghorofa Ubungo Kibangu na mabasi makubwa  kadhaa ambayo hutumika kuwasomba waumini bure kutoka Barabara ya Mandela hadi kanisani kwake.
Hivi karibuni Mzee wa Upako amewahi kuwakemea wachungaji wenzake wa makanisa ya kiroho kwa kujitajirisha kwa kujiita manabii na mitume akidai kwamba kufanya hivyo ni kuwatapeli waumini.

Range Rover Vogue.
“Inawezekana vipi mabomu yapigwe madhabahuni halafu wewe kama mtume na nabii usifanye jambo lolote la Kimungu dhidi ya waliofanya kitendo kile madhabahuni?” alihoji Mchungaji Lusekelo.
Alidai kuwa kuna mitume hapa nchini kazi yao ni kugombania ardhi. “Kama kweli wewe ni mtume na nabii halafu unagombania ardhi ya mashamba na Wazaramo, huo ndiyo utume tulioitiwa? Ndiyo maana hata serikali haitutambui,” alisema Mzee wa Upako huku akishangiliwa na waumini wake.
* MAGARI YANAYOONEKANA PICHANI JUU NI MIFANO YA MAGARI ANAYOMILIKI MZEE WA UPAKO. CHANZO CHA HABARI NI GLOBAL PUBLISHERS.

1 comment:

  1. Hahahahaaaa nimechekaje mie ....Safi sana Mzee wa Upako kwa kuikimbia laana ya Exemption ingawaje najua kwa aina ya magari uliyotaja...usingepata Exemption labda Ford Excape lipo chini ya CC 3000!!! Big Up!!!

    ReplyDelete

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate