EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, December 11, 2012

Waliopora wasindikiza maiti wanaswa.

JESHI la Polisi mkoani Singida, limefanikiwa kuwakamata watu 25 wanaotuhumiwa kuwa majambazi wakiwa na vitu vilivyoporwa kwenye gari la wafiwa lililokuwa limebeba maiti ya mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kwenda Tarime mkoani Mara.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida (ACP), Linus Sinzumwa, alisema kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa jana kufuatia msako mkali ulioendeshwa na askari polisi kwa kushirikiana na wananchi.

Alisema kuwa watuhumiwa hao wamekutwa na vitu mbalimbali walivyopora usiku wa kuamkia Jumamosi ya wiki iliyopita katika eneo la Kindai Manispaa ya Singida.
Sinzumwa alitaja mali zilizokamatwa kuwa ni pamoja na nguo za wasindikizaji, kadi mbili za ATM za CRDB, chaja mbili za simu, vitambulisho vya wafanyakazi hao, kamera, Laptop, simu, pamoja na sh 20,500 zizookotwa eneo la tukio.
Aliongeza kuwa pia watuhumiwa hao walikutwa na rungu nne na fimbo kadhaa vilivyotumika katika kuwapiga wafanyakazi hao wa SUA kabla ya kuwapora fedha sh milioni 10, simu za mkononi na mali zingine.

Kamanda alifafanua kuwa polisi bado wanaendelea kuwahoji watuhumiwa hao ili kubaini vinara wa tukio hilo kwani baadhi yao walikuwa wakijitapa kwenye vijiwe vya pombe kuwa na fedha za matumizi , huku wengine wakidai wanakula fedha za jeneza.
“Kwa sasa majina hatuwezi kuyataja maana bado tunaendelea na upelelezi na kuwasaka wengine na baadaye tutafanya upembuzi ili kuwabaini wale wahusika lakini pia nawaomba hawa wenzetu wa Tanroads kutoa mawe makubwa ambayo yapo pembezoni mwa barabara, ambayo wahalifu wanayatumia kuteka magari,” alisema.

Mwishoni mwa wiki iliyopita kundi la majambazi zaidi ya 10 yaliteka gari la SUA lililokuwa limebeba mwili wa marehemu mwanafunzi wa chuo na kupora fedha, simu za mikononi na vitu vingine kisha kuvunja jeneza na kumpekua marehemu.
Gari hilo aina ya Land Cruiser hard Top lenye namba za usajili SU 37012 lilikuwa likitotokea Morogoro kupeleka msiba wa mwanafunzi wa mwaka wa tatu Munchari Lyoba aliyefariki chuoni hapo, ambaye ni mkazi wa Tarime, mkoani Mara.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate