MALKIA wa mipasho, Khadija Kopa, amesema wasanii wa taarab hapa nchini ni wanafiki na ndio maana hata kuzikana inakuwa shida.
Khadija
Kopa aliyasema hayo jana Tandika, jijini Dar es Salaam, kwenye mazishi
ya mmoja wa wakurugenzi wa East African Melody, Lamania Shaaban.
Akiongea msibani hapo, Khadija Kopa ambaye ni mkurugenzi msaidizi wa
TOT, alisema inasikitisha sana kuona mtu muhimu kama Lamania anachangiwa
shilingi laki tatu na wana-taarab wenzake.
“Sisi
wasanii wa taraab ni wanafiki, hatupendani na hatutaki kuwa na umoja
wetu, tunashindwa na watoto wadogo wa Bongo Movie, tunadharaulika na
viongozi wa serikali kwa ajili ya ujinga wetu wa kukosa umoja.
Leo
hii akifa msanii wa Bongo Movie viongozi wengi wa vyama na serekali
wataonekana, sababu ni nini? Ni kwasababu wenzetu wana mshikamano.
“Tumekuwa tukijaribu kuhamasishana kuunda umoja lakini baadhi ya watu hususan wale wenye mafanikio wamekuwa wakituvunja moyo.
“Inasikitisha
sana kuona msiba wa msanii mmoja wa filamu ukihangaisha viongozi wa
kitaifa kuliko ajali ya Five Stars iliyoua zaidi ya wasanii 10 wa
taraab” alisema kwa uchungu Khadija Kopa.
Aliongeza:
“Umefika wakati sasa wa wasanii wa taarab kuungana, asiyetaka akae
kando ni bora tuwe na umoja wa watu wachache wenye moyo badala ya
kuwasubiri watu walioridhika na maisha yao, ni lazima sasa serikali
itambue kuwa Taarab ina umoja wao, ina sauti yao”
“Watu
wanaogopa kuwabeba wenzao walioko chini, hivi na sisi tusingebebwa
tungekuwa wapi? Pengine mimi ningekuwa Zanzibar naosha vyombo mpaka
makamo haya, nani angenijua” alihoji Khadija Kopa.
Khadija Kopa akiwasilisha mchango wake katika msiba wa Lamania
CHANZO SALUTI 5
No comments:
Post a Comment