EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, February 11, 2013

Chadema yawabana Makinda, Ndugai

VIONGOZI na mashabiki wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana walifanya maandamano na kuhitimishwa kwa mkutano wa hadhara uliofanyika Temeke, jijini Dar es Salaam ambako chama hicho kilitangaza nia ya kuandaa hoja ya kuwang’oa viongozi wa Bunge.
 

Hoja hiyo itawasilishwa katika mkutano ujao wa Bunge kwa ajili ya kuwapigia kura za kutokuwa na imani na Spika wa Bunge, Anne Makinda na Naibu wake, Job Ndugai kwa madai ya kukwamisha mijadala yenye masilahi ya wananchi bungeni.

Wakizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Temeke Mwisho, Dar es Salaam, wabunge wa chama hicho wakiwa na uongozi wa juu, waliwataka wananchi waliohudhuria mkutano huo kujiandaa na maandamano ya kuwang’oa spika hao.Kana kwamba hiyo haitoshi, wabunge hao walitangaza namba za simu za viongozi hao wa Bunge ili wananchi wazitumie kuwashinikiza wang’oke.


Akihutubia katika mkutano huo, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho (Bara), Zitto Kabwe alisema Spika Makinda ameshindwa kuwajibika na hivyo anapaswa kung’olewa kutokana na kutaka kuirudisha nchi kwenye kipindi cha kashfa ya Akaunti ya Madeni ya Nje ya Benki Kuu (Epa).

Akizungumzia kitendo cha Spika Makinda kuifuta Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Zitto aliyekuwa Mwenyekiti wa kamati hiyo alisema imefutwa kwa mbinu za CCM kuzima sauti ya wabunge wa upinzani wanaozungumzia masilahi ya wananchi.
Huku akishangiliwa na umati wa wananchi waliohudhuria mkutano huo, Zitto alitaja mbinu za kumng’oa Spika Makinda akisema kuwa hoja hiyo imeshakamilika.

“Kuna njia za kumng’oa Spika Makinda, kwanza kwa kupeleka hoja ya kutokuwa na imani naye na nimeambiwa hapa kwamba imeshakamilika. Au tuandamane hadi pale Shule ya Msingi Bunge… au tutumie namba zake kumpigia na kumtumia ujumbe wa simu za mikononi…” alisema Zitto na kumruhusu Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema kutaja namba za Spika Makinda na Naibu wake.
Baada ya kutaja namba hizo wananchi walionekana wakizipiga na wengine kutuma ujumbe wa simu.
Mwananchi lilipompigia simu Spika Makinda, simu yake ilikuwa inaita, kisha inakatika bila kupokewa.

Akizungumzia zaidi kuhusu kamati hiyo, Zitto alisema:
“Kamati hii iliundwa mwaka 2008 na aliyekuwa Spika Samuel Sitta kwa ushauri wa kina Dk Slaa (Willibrod, Katibu Mkuu Chadema), waliona kuwa haiwezekani nchi yenye zaidi ya mashirika 200 yenye thamani ya zaidi ya Sh10 trilioni yasidhibitiwe na Bunge…Lakini Serikali ya CCM ikaona upinzani umepata sehemu ya kuzungumzia, sasa wameifuta,” alisema Zitto.

Alitaja sababu ya kufutwa kwa kamati hiyo kuwa ni utendaji wa kamati hiyo uliogundua matumizi ya zaidi ya Sh1 trilioni kutoka kwenye mifuko ya pensheni zilizotumika katika kampeni za CCM ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Vyuo Vikuu vya Dodoma, Hombolo na Chuo Kikuu cha Arusha.

“Spika lazima ajue kwamba mamlaka yapo kwa wananchi na yeye ni msimamizi tu wa vikao vya Baraza la Wananchi liitwalo Bunge. Makinda lazima adhibitiwe, vinginevyo nchi yetu itaumia,” alisema Zitto.
Mnyika alia na Maghembe

Katika mkutano huo, Mnyika alitoa wiki mbili kwa Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe kuwa ameshughulikia matatizo ya maji kwa Jiji la Dar es Salaam.
Alisema kutokana na hoja aliyoiwasilisha katika kikao kilichomalizika mwishoni mwa wiki bungeni kuondolewa, analitaka Bunge lijadili na kupitisha maazimio ya hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa maji safi na ushughulikiaji wa majitaka katika Jiji la Dar es Salaam.

“Natoa wiki mbili kuanzia leo (jana) Waziri wa Maji (Maghembe) awe ameeleza hatua anazochukua kuhakikisha hali ya upatikanaji wa maji kwa Dar es Salaam,” alisema Mnyika na kuongeza:

“Asipofanya hivyo tutaandamana kwenda wizarani kwake kumshinikiza kutekeleza yale ambayo alisema yanaendelea,” alisema.
Awali akimkaribisha Mwenyekiti wa chama hicho, Dk Slaa alimtaka Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema kueleza hatua ambazo amefikia katika ufuatiliaji wa mabilioni yaliyofichwa nchini Uswiss.

Alisema watuhumiwa wa fedha hizo ndiyo vigogo katika Serikali, ndiyo maana hakuna jitihada zozote zinazofanyika kuhakikisha fedha hizo zinarudi.
Ahadi ya Mbowe

Akihitimisha mkutano huo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema kuwa ule mtindo wa wabunge wa chama hicho kususia vikao vya Bunge hautakuwepo tena badala yake wataendelea kupiga kelele ndani ya Ukumbi wa Bunge ili mikutano iahirishwe.

“Tulikuwa tunatoka nje ya Bunge, watu wakawa wanasema kuwa hatukuwachagua ili mkatoke nje, kwanza ni sawa na kumwachia nguruwe shamba la mahindi…Sasa hatutoki, tutakuwa tunakomaa na kupiga kelele hadi hoja zetu zisikilizwe… kama noma na iwe nomaa… kama noma na iwe nomaaa…” alisema Mbowe huku akishangiliwa na wananchi.
Kwa upande mwingine Mbowe aliilaumu Serikali kwa kukusanya kodi nyingi kila mwaka lakini haija
 
“Kwa kipindi cha Desemba 2011 hadi Desemba 2012 Serikali ya Rais Jakaya Kikwete imekusanya kodi ya Sh900 bilioni. Zote wanapeleka hazina, kisha wanakaa vikao Dodoma na kula na kustarehe. Watoto wetu wanashindwa kwenda shule…” alisema Mbowe na kuongeza:
“Kwa upande wa madini, asilimia 60 sawa na Sh256 bilioni iliyokusanywa kama kodi inatokana na wachimbaji wadogo kama ‘Pay as you earn’ (kwenye mishahara), wakati kampuni kubwa zimelipa Sh56,000 bilioni za kodi. Hivi wananchi mnasubiri nini? Mapambano haya hayatoshi bungeni tu, ndiyo maana tumekuja kwa wananchi hadi kieleweke.”
Mapokezi ya wabunge

Wabunge wa Chadema wakiongozwa na Mbowe walipokelewa majira ya saa nne asubuhi ambapo magari ya chama hicho na idadi kubwa ya wakazi wa Dar es Salaam walijikusanya kwa ajili ya kujiunga na msafara ulioanzia maeneo ya Riverside, Ubungo mpaka Uwanja wa Temeke Mwisho.

Shamrashamra za kuwapokea viongozi hao, zilifanyika mpaka majira ya saa 7.00 mchana baada ya kuwasili katika eneo hilo tayari kwa msafara wa kuelekea kwenye uwanja huo.
Magari zaidi ya 70 yaliyokuwa kwenye msafara huo yaliyokuwa yamefurika katika Barabara ya Mandela kwa takriban saa tatu huku magari ya John Mnyika, Tundu Lissu, Zitto Kabwe na Godbless Lema yakivamiwa kwa furaha na wakazi hao katika kona ya kuingia Tandika.
Imeandikwa na Elias Msuya, Kelvin Matandiko, Ibrahim Yamola-Mwananchi    
     

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate