EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, February 10, 2013

Makinda atumika kumfuta Sitta

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda na Naibu Spika, Job Ndugai, wanasemekana kutumiwa na maadui wa demokrasia na mafisadi kummaliza kabisa aliyekuwa Spika wa Bunge hilo, Samuel Sitta na kundi lake.

Habari za kuaminika kutoka vyanzo mbalimbali zimebainisha kuwa kile kilichotokea bungeni na kusimamiwa kikamilifu na Makinda ulikuwa ni utekelezaji wa matakwa ya wanasiasa na viongozi kadhaa wenye nguvu za fedha ambao waliumizwa vibaya na aina ya uongozi na maamuzi ya Sitta alipokuwa akikalia kiti hicho.
Inadaiwa kwamba mbali na kumkomoa, Makinda pia ameelekezwa kuhakikisha kuwa Sitta anamalizwa kisiasa, kwa kuwasulubu pia wabunge waliokuwa wakimuunga mkono, wakiwamo wale wa vyama vya upinzani hususan wa CHADEMA.

Moja ya chanzo chetu cha habari kimesema kuwa wanasiasa hao wakiwamo watendaji kadhaa wa serikali, walichukizwa na msimamo wa Sitta, hasa kusimamia ukweli na haki, na kuonekana kuwapendelea zaidi wabunge wa upinzani kuliko wale wa CCM.

Katika mkakati huo, iliamriwa kuwa nguvu zote alizotumia Sitta kuisulubu serikali na wanasiasa walioguswa masilahi yao, zivunjwe, likiwamo suala la kuunda na kuunganisha kamati ya hesabu za mashirika ya umma, na ya hesabu za serikali kuwa pamoja, kisha kuhakikisha inaongozwa na mbunge kutoka chama tawala.
Mbali na mipango hiyo, chanzo chetu kimesema kuwa mabadiliko hayo ya kamati yamefanywa kutokana na hofu ya kuumbuka kwa serikali kutokana na matumizi mabaya ya fedha, ikiwa kamati hizo zitaendelea kuwa chini ya wapinzani.

Katika mpango huo, Naibu Spika Ndugai, amejikuta akilazimika kukubaliana na maagizo ya mkuu wake wa kazi, licha ya ukweli kwamba ndiye alikuwa mwenyekiti wa kamati maalumu iliyoundwa katika Bunge la Tisa lililoongozwa na Sitta, ikiwa na lengo la kuleta mfumo mzuri wa utendaji wa Bunge, ikiwa ni pamoja na kurejesha hadhi yake ya kuiwajibisha serikali.

Ndugai katika kukamilisha azima ya Sitta, alilazimika na kamati yake iliyoundwa na wabunge wengine, Dk. Harrison Mwakyembe, Nimrod Mkono, Beatrice Shelukindo, Dk. Willibrod Slaa na Hamadi Rashid Mohamed, ilifanya ziara katika Bunge la Kenya, Uganda, India, Mauritius na Zimbabwe.
Kutokana na ziara hizo za mafunzo, Ndugai na kamati yake walipendekeza kutungwa kwa mambo yatakayolifanya Bunge lisimamie masilahi ya taifa badala ya vyama, vikao vyake kuoneshwa wazi kwa njia ya runinga ili wananchi waone na ripoti za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali zijadiliwe na Bunge pamoja na kuondoa miswada yoyote iliyokuwa inaletwa kwa dharura bungeni.
Ni kamati ya Ndugai ndiyo ilipendekeza kuwa Kamati ya Mashirika ya Umma, (POAC), Kamati ya Serikali za Mitaa (LAAC) na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) ziongozwe na upinzani ili kuongeza uwajibikaji wa serikali kwa Bunge.

Mbunge mmoja wa CCM ambaye amekuwa bungeni kwa muda mrefu (jina linahifadhiwa) alikiri kusikitishwa na uamuzi wa Spika Makinda, na kuonesha hofu ya kuvunjika kwa heshima na hadhi ya Bunge.
“Inasikitisha sana, maana sasa tunaelekea kuvunja hadhi ya Bunge na kulinda uozo wa serikali.
“Katika Bunge la Tisa, Sitta alijitahidi kuwa jasiri, kutopindisha ukweli ili kuilinda serikali, na alizielewa vizuri kanuni hasa ile ya 8 inayosema: “Hata kama Spika ametoka katika chama fulani anapaswa atende haki kwa pande zote,” alisema mbunge huyo.

Mbunge huyo alisema vurugu zilizotokea bungeni zilitokana na maamuzi mabaya ya kiti cha Spika, kinyume kabisa cha hotuba yake ya kwanza alipochaguliwa kushika wadhifa huo ya kuliunganisha Bunge kuwa moja.
Wakizungumza na Tanzania Daima Jumapili kwa njia ya simu, mmoja wa wajumbe wa iliyokuwa kamati ya Ndugai, Nimrodi Mkono, alisema hawezi kusema lolote kuhusiana na kuondolewa kwa kamati hizo, ingawa alikiri kuwa walichokishauri na kukubaliwa na Bunge kilikuwa cha maana na manufaa kwa taifa.
Kuhusiana na vurugu zilizotokea, Mkono alisema kelele za wapinzani zilikuwa sahihi hasa baada ya kuona kuwa wanaonewa, kutokana na uchache wao, hivyo kulazimika kupiga kelele ili hoja zao zisikiwe na Watanzania.

Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed, alishangaa kuunganishwa kwa Kamati ya Mashirika ya Umma pamoja na ile ya Hesabu za Serikali, huku akihoji kama Spika na wabunge wa CCM wapo tayari kuwa na mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti kutoka upinzani.
Akihojiwa kwa sharti la kutotajwa jina gazetini, kiongozi mmoja mashuhuri hapa nchini, amelaani aliouita uendeshaji mbovu wa shughuli za Bunge, na kuongeza kuwa kumetokana na udhaifu wa serikali yenye wabunge wasiojali masilahi ya taifa.
Alikwenda mbali zaidi na kudai kuwa kauli ya hivi karibuni ya Makinda wakati akitoa maoni mbele ya wajumbe wa kamati ya kukusanya maoni ya Katiba, ya kutaka Spika atoke nje ya chama, ilionesha kuwa huenda hata yeye analazimika kutekeleza maagizo na maelekezo ya chama na serikali yake hata kama hayataki.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate