.jpg)
Mwanafunzi 
 wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Tegeta jijini Dar es 
Salaam, Bertha Amir (14), pichani, amejinyonga hadi kufa akipinga 
kulazimishwa na mama yake mzazi kusoma.
Kamanda
 wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura, alisema mwanafunzi huyo 
alijinyonga juzi  saa 11:00 jioni, maeneo ya Tegeta Namanga, jijini Dar 
es Salaam.
Alisema marehemu alikutwa amejinyonga chumbani kwa kutumia mtandio ulioning’inizwa juu ya dari.
Kamanda
 Wambura alisema sababu za mwanafunzi huyo kujinyonga bado 
hazijafahamika, lakini akasema inasadikika kuwa wakati wa enzi za uhai 
wake, siku moja kabla ya kifo chake, alikuwa ameongea na mama yake, 
Angelina Maiko Mshami (30), ambaye alimtaka achukue fedha kwa ajili ya 
kujiandaa kwenda shule.
Kamanda
 alisema kuwa mwili wa mwanafunzi huyo umehifadhiwa katika Hospitali ya 
Mwananyamala kwa uchunguzi na kwamba, polisi wanaendelea na upelelezi 
kuhusiana na kifo chake.
 Mama
 wa mtoto huyo, Angelina Mshami, alisema alishangazwa na kitendo cha 
mtoto wake kuamua kukataa shule ghafla wakati alikuwa ana uwezo mzuri 
darasani.
Alisema
 kuwa mtoto wake alikuwa na akili darasani akishika nafasi ya kwanza ama
 ya pili wakati akisoma shule ya msingi na hivyo kumfanya afaulu 
kujiunga  kidato cha kwanza.
Hata hivyo, alisema kabla ya kifo chake, binti yake alimweleza kuwa hataki shule bali anataka kufanya kazi.
Alisema alipomuuliza kazi gani anataka kuifanya, hakuitaja bali alisisitiza kuwa anaifahamu mwenyewe.
Betha ambaye ni mtoto wa kwanza kati ya watoto wawili katika familia yao, alizaliwa mwaka 1999, Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga.
Alianza 
 darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Malindi mkoani Tanga na 
kufanikiwa kujiunga na Shule ya Sekondari Mtumbi na baadaye kuhamishiwa 
katika Shule ya Sekondari Tegeta.
Aidha, baadhi ya majirani waliokuwapo msibani hapo, walielezea masikitiko yao na huzuni kuhusiana na kifo cha msichana huyo.
Marehemu anatarajiwa kusafirishwa leo kuelekea mkoani Tanga kwa mazishi yatakayofanyika kesho kijijini Malindi
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment