EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, October 10, 2013

Mgomo wanukia Simba..Henry Joseph atoswa kambini.

WACHEZAJI wa Simba wakiwa kwenye mgomo baridi kushinikiza kuondolewa kwa Kocha Msaidizi Jamhuri Kihwelo ‘Julio,’ kiungo Henry Joseph ametemwa kwenye kikosi cha timu hiyo kilichoingia kambini Bamba Beach, juzi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam kujiandaa na mechi za Ligi Kuu.

Habari kutoka ndani ya klabu hiyo, zinasema kuwa, chanzo cha kuachwa kwa Henry ni baada ya kusigana na Julio tangu Jumatatu wiki hii wakati wa mazoezi kwenye Uwanja wa Kinesi, ambapo nyota huyo aligomea mazoezi.

Kuna habari kuwa, Henry alipoulizwa ni kwanini alikuwa kwenye hali ya kusuasua, akajibu kuwa tayari alishajifua kivyake, jibu ambalo lilimkera Julio na kumtaka aondoke uwanjani hapo, hivyo kutojumuishwa kambini.

Tanzania Daima ilipojaribu kutafuta kiini cha msigano ndani ya timu hiyo, baadhi ya wachezaji walikiri Henry kusigana na Julio na kuongeza kuwa, kuna mgomo baridi unaotokana na wao kukerwa na kocha huyo msaidizi.

Chanzo hicho kilidokeza kuwa, Julio amekuwa akichukiwa na wachezaji kutokana na lugha zake za karaha na matusi, ambazo zimekuwa zikiwanyima raha wachezaji dimbani hasa kwenye mazoezi.

“Hali sio nzuri katika timu yetu, mpaka sasa Henry hayupo kambini baada ya kutokea mabishano baina yake na Julio, tukiwa mazoezini Jumatatu,” alisema mmoja wa wachezaji wa timu hiyo ambaye hakupenda kutajwa jina.

Alipotafutwa Ofisa Habari wa klabu hiyo, Ezekiel Kamwaga, alisema hajui lolote kuhusu suala hilo na kama kuna ukweli, bado ni suala la kiutendaji zaidi linalohitaji kufanyiwa uchunguzi zaidi kabla ya kutolewa majibu kwa maslahi ya Simba.

Juhudi za kumpata Julio kutoa ufafanuzi wa kilichotokea kati yake na Henry, ziligonga mwamba kwani licha ya kutafutwa mara kadhaa kwa siku ya jana, simu yake haikuwa hewani.CHANZO NI TANZANIA DAIMA.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate