EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, January 19, 2013

Msigwa aifyatua Ikulu.. Aituhumu kuwapa vyeo majangili

Habari na Abdallah Khamis na Lucy Ngowi
BAADHI ya maofisa wa taasisi nyeti za serikali ikiwemo Ikulu, wametuhumiwa kula njama kuwaficha watu waliotuhumiwa kuhusika na vitendo vya ujangili na wengine kuwapandisha vyeo vikiwemo vya ubalozi.

Tuhuma hizo zimetolewa jana na Waziri Kivuli wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mchungaji Peter Msigwa, alipozungumza na waandishi wa habari na kueleza kusudio lake la kupeleka hoja binafsi bungeni ili kuunda tume ya kuchunguza sakata zima la tuhuma za ujangili.

Hata hivyo, mbunge huyo hakuweza kutaja majina ya maofisa wanaotuhumiwa, lakini akafafanua kuwa alipokuwa katika kamati ndogo ya kufuatilia utoroshwaji wa twiga, kuna majina ya watu yalitajwa kwa ajili ya kuchunguzwa na ikibidi wachukuliwe hatua, lakini kilichofanyika ni wahusika kupewa vyeo vya utumishi, ukiwemo ubalozi.
Msigwa alisema tayari Januari 8 mwaka huu katibu wa Bunge amemtaka awasilishe maelezo ya hoja yake kwa Spika kufuatia barua aliyoandika Desemba mwaka jana juu ya dhamira ya kuwasilisha hoja binafsi.

“Nitaomba iundwe kamati teule ya Bunge kufuatilia huu ujangili unaoendelea nchini, kwani tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa robo ya pembe na meno ya faru na ndovu duniani zinatoka Tanzania.

“Idadi ya tembo wanaouawa ni wastani wa 67 kwa siku, na hali hiyo ni hatari kwa rasilimali asili za taifa na pia inahatarisha maliasili na urithi wa nchi,” alisema.
Alisema mtandao wa ujangili nchini ni mkubwa kuliko inavyofikiriwa, na kwamba hata wanaojitoa mhanga kushughulikia hali hiyo maisha yao yanakuwa hatarini.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, alipoulizwa juu ya tuhuma hizo, alikana kuhusika kwa Ikulu, lakini akadai kuwa mtandao wa biashara hiyo ni mkubwa, na kwamba mazingira yaliyopo yanatia shaka kuwa baadhi ya viongozi wanahusika.

“Haiwezekani kontena linapitishwa bandarini Dar es Salaam bila mtu yeyote kujua nini kimebebwa, halafu ufike Indonesia au China ndipo pembe hizo na meno yakamatwe, kuna kuzembea hapo na rushwa ndani yake,” alisema.
Alikiri kudokezwa na Mchungaji Msigwa kuhusu kusudio la kupeleka hoja binafsi na kudai kuwa ni hatua nzuri inayotokana na ukereketwa na uzalendo alionao kwenye rasilimali za taifa.

Hata hivyo, Kagasheki alisema idadi ya tembo inayotajwa kuuawa nchini si ya kweli kwa kuwa juhudi za udhibiti zinazofanywa na wizara yake zimepunguza kasi hiyo hadi kusifiwa na Jumuiya ya Ulaya.

“Hizi pembe za ndovu zinazokamatwa si kwamba tembo wote wameuawa wakati huu, haya ni makusanyo ya muda mrefu huko nyuma. Lakini vile vile watu wanapaswa kuelewa kuwa tembo wengi si kweli kuwa wanauawa Tanzania,” alisema.
Kagasheki alisema kuwa pembe hizo na meno ya tembo yanatoka kwa wingi katika nchi za Malawi na mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambako wanyama hao wanauawa zaidi, lakini usafirishaji wake unapitia katika bandari ya Tanzania.
Alisema nchi hizo hazina bandari na hivyo hutumia Tanzania hali inayofanya nyara hizo zinapokamatwa nje ya nchi kuonekana kuwa zimetoka hapa, hivyo kuonekana kama kitovu cha biashara hiyo.

Lembeli apigilia msumari
Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira imepigilia msumari kwa kuanika namna hoteli za kitalii zilivyoongoza kwa hujuma.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, James Lembeli akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam jana, alisema wamiliki wa hoteli hizo wamekuwa wakiilipa serikali dola 4 tu, kwa kila mgeni wanayempokea, wakati wao wamekuwa wakitoza dola 350.
Lembeli alisema hujuma hiyo, imetokana na mikataba ya ovyo iliyopo, na hivyo akaagiza serikali kuwasilisha mikataba yote ya hoteli zilizoko ndani ya hifadhi, kuchunguza kwanini zinalipa kiasi kidogo cha fedha ilhali wanakusanya zaidi.
Lembeli alisema kumekuwepo na mzozo na malumbano katika hoteli za Ngorongoro, Seronera na Noro, ambazo kwa mujibu wa mikataba iliyopo pesa inayolipwa dola 4 ya kila mgeni kwa siku ni ndogo.
“Tulipowahoji walisema kuwa mikataba inawafunga. Je, ni kwanini watu hawa wanatengeneza pesa ndani ya hifadhi, lakini hawachangii kile wanachokipata?” alihoji Lembeli.
Alisema kuna mchezo mchafu unafanywa ndiyo maana zilitolewa kwa bei ya kutupwa, kiasi kwamba kama Mwalimu Julius Nyerere angefufuka leo na kushuhudia ufisadi huo angetoa machozi.
Alishangaa kuona kuwa, mtu anayeweka ‘tenti’ ndani ya hifadhi analipa dola 60 kwa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa nchini (Tanapa) iweje hoteli hizo kubwa zilipe dola nne mpaka sita?
Katika hatua nyingine, Lembeli amemshukia Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wassira kwamba ndiye tatizo kubwa la wananchi kuishi katika maeneo ya malisho ya wanyama.
Lembeli aliyasema hayo jana mbele ya Waziri Kagasheki na Naibu wake Lazaro Nyalandu wakati wa kujadili ripoti ya wabunge wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira.
Alisema Wassira ni tatizo na amemtaka kukaa naye ili wananchi katika jimbo lake waache kuingia katika maeneo ya Ushoroba ambayo ni sehemu sahihi ya malisho ya wanyama katika hifadhi hizo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate